Zinazobamba

HATMA YA YUSUF MANJI NI OCTOBA 6,SOMA HAPO KUJUA

Mahakama ya Hakimu ya Mkazi Kisutu, imepanga Oktoba 6, mwaka huu kutoa  hukumu katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Yusuf Manji(41).

Uamuzi huo umetolewa leo na Hakimu Mkazi Mfawidhi , Cyprian Mkeha, baada ya wakili wa utetezi Hajra Mungula kusema kuwa ameshafunga ushahidi wa mashahidi saba.

Mashahidi watatu wa upande wa mashtaka wametoa ushahidi wao dhidi ya mshtakiwa Daktari Mfawidhi wa Gereza la Keko, Inspekta Eliud Mwakawanga ameileza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jinsi maisha ya mfanyabiashara Yusufu Manji yalivyo kuwa gerezani kwamba alikuwa akitumia vidonge kati ya 25 mpaka 30 kwasiku.

Ameeleza kwamba  walikuwa wakimpatia dawa hizo alipokuwa akisikia maumivu hasa ya mgongo na kwamba kuna kipindi alikuwa anaamka akiwa na hali ya kutetemeka au kuchanganyikiwa.

Ameeleza kuwa Julai 6, 2017 walimpokea Manjia kitokea Hospitali ya Muhimbili Kitengo cha Moyo cha JKCI ambapo waliambiwa ni mshtakiwa lakini ni mgonjwa.

“Nilienda kumuona, tukazungumza naye na tulikaa naye gerezani hadi alipokuja kuachiwa,”