BAADA YA SERIKALI YA JPM KULIFUNGIA GAZETI LA RAIA MWEMA, HASHIM RUNGWE AIBUKA NA KUI "POPOA " SERIKALI,SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
WAKATI ndani ya siku kumi serikali ya Rais ya John Magufuli ikiwa ni teyari imeyafungia magazeti mawili ndiyo naweza kusema baada ya leo serikali kutangaza
kulifungia kwa siku 90 gazeti linalotoka mara moja kwa wiki la Raia Mwema
kutokana na kuandika habari inayodaiwa inayomchafua Rais Magufuli.
Mbali na Gazeti hilo katika siku hizo, pia serikali hiyo imetangaza kulifungia kwa miaka miwili gazeti la Mwanahalisi kutokana na
kuandika habari ambazo serikali inadai zinakiuka kanuni za uandishi wa habari.
Hatua hiyo imepingwa vikali na wanasiasa huku wakisema hatua
hiyo ni muendelezo wa serikali ya Rais Magufuli kuminya demokrasia .
Hashim Rungwe (Pichani) ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Ukombozi wa
Umma ameumbia Mtandao wa Fullhabari.blog, kuwa hatua ya serikali kulifungia gazeti hilo imekiuka msingi ya haki za binadamu huku akitaja ni mwendelezo wa ukandamizaji wa demokrasia hapa nchini.
“Huu ni muendelezo wa ukandamizaji wa demokrasia,ameaanza kwetu wanasiasa,Leo
wanataka kuwatisha wanahabari wasiandike habari
ambazo wa wao hawasipendi,”amesema Rungwe.
Rungwe ambaye alikuwa mgombea wa Urais kwenye uchaguzi mkuu
wa mwaka 2015 amesema kwa sasa kinachoonekana kwenye tasnia ya habari ni
serikali kujivika koti Uhariri wa habari.
"Sahivi serikali imekuwa mhariri wa habari,kama utaki watu waandike habari si useme waandike za kukusifia wewe,akumbuke yeye ni baba wafamilia lazima watu wamkosoe,"amesema Rungwe ambaye ni Wakili Msomi.
"Sahivi serikali imekuwa mhariri wa habari,kama utaki watu waandike habari si useme waandike za kukusifia wewe,akumbuke yeye ni baba wafamilia lazima watu wamkosoe,"amesema Rungwe ambaye ni Wakili Msomi.
Mwenyekiti wa Bodi ya Raia Mwema, Jenerali Ulimwengu amesema wameambiwa sababu ya kusitishwa kwa gazeti hilo ni habari hiyo.
Ulimwengu amesema kwa sasa wanashauriana kuona ni nini cha kufanya.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Idara ya
Habari maelezo,Dk Hassan Abbasi kwa vyombo vya habari inasema serikali imefikia
hatua kulifungia gazeti la Raia Mwema kutokana kuandiika nukuu ya uongo kwa
Rais Magufuli.
Amesema toleo la namba 529
la terehe 27 semptemba hadi Oktoba mwaka ilichapisha habari ya Uchambuzi
inayosema “URAIS UTAMSHINDI JOHN MAGUFULI”
“Makala hiyo ilisheheni
nukuu za kutunga na zisizo za ukweli
zikimsingizia Rais John Magufuli ,Gazeti hili limeonywa sana huko nyuma
dhidi ya uandishi wake” Amesema
Kufungiwa kwa Gazeti hili kunakuja ni siku moja baada ya
wamiliki wa Gazeti la Mwanahalisi kutangaza kukimbilia Mahakamani kutaka Gazeti
hilo lifunguliwe.
Kufungiwa kwa Gazeti la Raia Mwema linakuwa ni miongozi mwa magazeti zaidi ya 400 kufungia tangia Rais Magufuli aingie madarakani katika miaka yake miwili,
]Magazeti 400 hayo mengi yake yakifungiwa kutokana na kutochapishwa kwa mada mrefu huku yaliobakia yakifungiwa kwa sababu inayotajwa kuwa yanakiuka misingi ya uandishi wahabari.
]Magazeti 400 hayo mengi yake yakifungiwa kutokana na kutochapishwa kwa mada mrefu huku yaliobakia yakifungiwa kwa sababu inayotajwa kuwa yanakiuka misingi ya uandishi wahabari.