Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul
Makonda ametimiza ahadi zake kwa kwa jamii, taasisi, watendaji na watu
binafsi kufuatia ziara yake ya Dar Mpya iliyoanza Novemba 18 mpaka 28
ambapo alikutana na kero mbalimbali zilizohitaji ufumbuzi ili kuondoa
changamoto kwa makundi hayo tajwa.
RC Makonda amekabidhi vifaa mbalimbali
kwa waliohaidiwa vyenye thamani ya shilingi milioni 164,272,000 ambapo
kwa upande wa kituo cha kulea waathirika wa dawa za kulevya kilichopo
Kigamboni kinachoitwa Pedderef House of Wisdom RC Makonda amewapatia
jiko la gesi, mitungi miwili ya gesi, king’amuzi, luninga na magodoro
50.
Pia kutokana na utendaji mwema wa
watendaji wa mitaa na wenyeviti RC Makonda amemkabidhi Mtendaji wa Kata
ya Buyuni pikipiki 1 na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Buguruni piki
piki 1, huku kwa watumishi wanne ambao utendaji wao umedhihirisha hali
yao ya utayari wa kujitolea na kufanya kazi kwa ufanisi wa hali ya juu
ambao amewazadia watumishi kulala katika Hoteli ya Kilimanjaro ambao ni
Dr Grace Magembe, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Mruto
Kamanda Polisi Mkoa wa Temeke, Edward Otieno Katibu Tawala Msaidizi
Uchumi na Uzalishaji Sekretarieti ya Mkoa na Aron Joseph Mkurugenzi wa
Uendeshaji DAWASCO.
Kuhusu suala la ujasiriamali RC Makonda
amekabidhi Milioni Moja kwa kijana Evans Tulizo wa Soko la Sterio
Temeke, pia amempatia kiasi cha shilingi laki mbili mjasiriamali mdogo
kwa ajili ya biashara yake ya machungwa, kuhusu changamoto ya maji RC
Makonda amemkabidhi Mstahiki Meya Manispaa ya Ilala Charles Kuyeko cheki
ya shilingi milioni 13 ili wananchi wa Gongo la Mboto na Pugu waweze
kupata Maji na kuiondoa changamoto iliyokuwa inatokana na ubovu wa
miundombinu, huku akiongeza kiasi cha shilingi laki tano ikiwa ni
mchango kwa ajili ya kukamilisha ununuzi wa tanki la maji kwa wananchi
wa Buyuni na kata ya Pemba Mnazi.
Kwa upande wa kuunga Mkono ujenzi na
ukarabati RC Makonda amekabidhi mabati 2000 katika shule ya Sekondari
Jitegemee huku shule ya Msingi Mbagala Annex ikikabidhiwa mabati 1000,
Shule ya Katoliki ikikabidhiwa mifuko 1000 ya saruji, Matofali 10000 kwa
ajili ya kanisa la AIC, Mabati 300 kwa ajili ya Soko la Samaki Msasani,
Mabati 200 kwa ajili ya uwanja wa Taifa, Tumba kwa ajili ya kwaya ya
JWTZ na gari la kubebea wagonjwa kwa Polisi FFU Ukonga na msaada wa
fedha za matibabu wenye jumla ya shilingi milioni nne kwa watu
mbalimbali hususani wazee na kina mama.
Huku kwa upande kamanda kanda maalumu
ya Dar es salaam Stanley kabiki ametoa shukrani zake kwa RC Makonda
baada ya kupatiwa msaada wa gari la kubebea wagonjwa ambalo lilikuwa ni
changamoto kubwa kwa upande wao kwa kipindi kirefu kwa wanahudumia
wakazi wengi ikiwemo wanaotokea Msongola na Chanika, huku akihaidi
watalitumia bila ubaguzi wowote.
Jiunge
TUKIO KUBWA ALILOFANYA RC MAKONDA,SOMA HAPO KUJUA
Reviewed by Unknown
on
19:51:00
Rating: 5