DC HAPI AWAANGUKIA MAWAKALA WA MISUTU,SOMA HAPO KUJUA
Mkuu
wa Wilaya ya Kinondoni Ali Salum Hapi amewaomba Wakala wa Misitu nchini (TFS)
kumsaidia mbao kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa 1068 kwa shule
zilizopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondon
Mkuu
wa Wilaya ya huyo ameyasema hayo wakati akipokea msaada wa madawati 80 yenye
thamani ya shilingi milioni tano na laki sita kutoka kwa Wakala wa Misitu
nchini kanda ya Kinondoni.
DC
Hapi ameeleza kuwa wilaya yake imemaliza tatizo la madawati hata waliyoyapokea
leo ni ziada tu, hivyo ametumia fursa hiyo kumuomba Meneja wa Wakala wa Misitu
Alex Mbaga kuwasaidia mbao kwaajili ya ujenzi wa madarasa kwa kuwakea milango
na madirisha kwani tayari wamepokea msaada wa saruji na mabati yav kutosha kwa
ajili ya vyumba hivyo mbao hizo zitawasaidia kurahisisha kazi.
Hapi ameongeza kuwa katika kipindi
hiki kifupi wameweza kujenga shule mbili ambazo fedha za ujenzi huo zimetokana
na mchango wa Rais Dkt John Pombe Magufuli.