Zinazobamba

YESU, IMAM HUSEIN WANAFANANA KWA HAYA

Kiongozi Mkuu wa kiroho wa Waislam wa dhehebu la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh HEMED JALALA  akizungumza na wanahabari mapema Leo Jijini Dar es salaa.
Imeelezwa kuwa Yesu na Imaam Husein (Mjukuu wa Mtume) wanafanana kwa harakati zao za kuamrisha mema, kukatazana maovu jambo ambalo kila mmoja alijitoa kuhakikisha mema yanatendeka ili dunia kuwa sehemu salama ya Kuishi.
 Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Kiongozi Mkuu wa kiroho wa waislam wa dhehebu la Shia ITHNASHERIYA Tanzania Sheikh HEMED JALALA  wakati wa semina maalum kwa ajili ya kujadili kwa pamoja Jitihada za wawili hao katika kuleta Amani na utulivu pamoja na kuleta haki na usawa Duniani.
 
Sheikh Jalala amesema watu hao ni mfano wa kuigwa kwa sasa hii ikiwa ni semina pia ya kuadhimisha Arobaini ya Mjukuu huyo wa mtume Mohamad (s.a.s)

Sheikh Jalala amesema kuwa Semina hiyo inalengo la kuweka ulinganisho kwa watu hao wawili ambao ni Imam Husein na Nabii Isaa ambaye ni Yesu ambao wote kwa pamoja walikuja Duniani kwa ajili ya kuleta mabadiliko kwenye Dunia katika Nyanja mbalimbali zikiwemo Haki kwa watu wote,na kutetea wanyoonge na kufanya watu wapendane katika Jamii.


Semina Ikiendelea
Ameongeza kuwa ni wakati wa watanzania kuacha mambo mambo mabaya na kuanza kufanya matendo ya kiumpendaza mungu yakiwemo kupendana,kupinga dhuluma,na kutetea wanyonge ili kuhakikisha kuwa wanawaenzi viongozi hao wa Kidini waliopambana kwa ajili ya dunia.
Picha mbalimbali za semina Hiyo ---