WANAFUNZI WA KIDATO CHA PILI WAANZA MITAHANI YAO LEO,PIA SERIKALI YAFAFANUA UKWELI WA KUFUTWA KWA DIPLOMA YA UALIMU,SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
Jumla ya wanafunzi 435,221wa kidato cha pili nchi
nzima leo wametarajia kuanza mitihani yao ya taifa ya kidato cha pili.
Ambapo kati yao wavulana ni 214,013 sawa na asilimia 49.17 na wasichana 221,208 sawa na asilimia 50.83.
Ambapo kati yao wavulana ni 214,013 sawa na asilimia 49.17 na wasichana 221,208 sawa na asilimia 50.83.
Mbali na hao wapo wanafunzi wenye mahitaji maalum
ambao watahiniwa wasioona ni 67 na watahiniwa wenye uoni hafifu ni 306 ambao
watapewa maandishi ya karatasi hukuzwa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es
salaam.
Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani nchini,Dkt Charles Msonde amesema mtihani huo ambao umeanza mapema hii leo ambao unatarajia kumalizika Nombemba 25 ya mwaka huu.
Katibu mkuu wa Baraza la Mitihani nchini,Dkt Charles Msonde amesema mtihani huo ambao umeanza mapema hii leo ambao unatarajia kumalizika Nombemba 25 ya mwaka huu.
Amesema mtihani huo unalengo la kuwapima uwezo na uelewa kwa wanafunzi katika yote wajifunzayo kwa miaka miwili ya masomo yao huku wanafunzi wanaofeli wanakosa nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu.
Dkt Msonde amesema maandalizi yote ya mtihani huo
yamekamilika ikiwemo kusambazwa kwa mitihani itakayotumika katika upimaji huo
pamoja na nyaraka muhimu katika mikoa na halmashauri zote ndani ya Tanzania
bara.
Hata hivyo,Dkt msonde amesema Jumla ya wanafunzi
10,045,99 wanatarajia kuanza mitihani ya darasa la nne mwaka huu siku ya tarehe
23 na 24 Novemba ambapo kati yao wavulana ni 507,732 sawa na asilimia 48.54 na
wasichana na 538,267 sawa na asilimia 51.46.
Pamoja na hayo dkt msonde amewataka wanafunzi pamoja na wasimizi kutohusika na vitendo vya udanganyifu huku akisema hatua kali za kisheria kwa waliohusika
Pamoja na hayo dkt msonde amewataka wanafunzi pamoja na wasimizi kutohusika na vitendo vya udanganyifu huku akisema hatua kali za kisheria kwa waliohusika
Pamoja na
hayo Dk Msonde amefafanua kuwa mafunzo ya
ualimu wa shule ya msingi ngazi ya stashahada yamefutwa lakini wanafunzi
waliopo vyuoni watamalizia masomo yao kwa muda uliobaki.
Dk Msonde
amesema mafunzo hayo ya walimu yataendelea kwa utaratibu wa zamani ambao
ulikuwa ngazi ya cheti.
Amesema
usimamizi wa mitihani hiyo itakuwa chini ya Necta kama ilivyokuwa zamani badala
ya Nacte.
"Wanafunzi
walio vyuoni wataendelea na mafunzo hayo, isipokuwa kuanzia mwaka huu
hatutadahili kwa ngazi ya diploma, tutadahili ngazi ya cheti kama ilivyokuwa
zamani," amesema Dk Msonde.