Zinazobamba

RAIS MSTAAFU KIKWETE KUWATUNUKU SHAHADA MBALI MBALI WAHITIMU WA UDSM KESHO,YUMO PIA MZEE MBEKI,SOMA HAPO KUJUA


Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dk. Jakaya Mrisho Kikwete kesho anatarajiwa kumtunuku shahada ya Heshima ya Udaktari ya chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM)mpigania uhuru na mwanaharakati mashuhuri ambaye ni Rais mstaafu wa Jamhuri ya Afrika Kusini Thabo Mbeki.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Mbali na Kiongozi huyo,Pia Kikwete anatarajiwa kuwatunuku shahada mbali mbali watahitimu 6717 ambao wamemaliza masomo yao katika chuo hicho,

Ambapo kati yao kati yao 61 wanatunukiwa Shahada ya Uzamivu, 627 Shahada za umahiri na 59 Shahada ya Uzamili huku wahitimu 5968 Shahada za awali.
Profesa  Rwekeza Mukandala ambaye ni Makamu mkuu wa chuo UDSM amewaamia waandishi wa habari kuwa amesema kuwa Mahafali hayo yataenda sambamba na kusimikwa rasmi kwa Dk. Jakaya Kikwete kuwa Mkuu mpya wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
 Profesa Mkuandala amesema Mbeki amekubali kupokea tuzo hiyo ya heshima na atahudhuria awamu ya kwanza ya mahafali ya 46 ya Chuo kikuu cha Dar na anatunukiwa tuzo hiyo kutokana na mchango mkubwa na wakipekee katika kupigania haki bara la afrika