PROFESA MUKANDALA AAGA RASMI UDSM,SOMA HAPO KUJUA
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),
Profesa Rwekaza Mukandala, ameiaga rasmi jumuia ya Chuo hicho baada ya
kukitumikia kwa miaka 10, tangu 2006 alipoteuliwa kushika wadhifa huo.
Sehemu ya hotuba yake kwenye mahafali ya 46 ya chuo
hicho leo, Dar ilisema, "Nimekitumikia chuo hiki kwa miaka 10, leo hii ni
mahafali yangu ya mwisho kuhudhuria kama Vice Chancellor wa UDSM, muda mfupi
umebaki nipumzike nimpe kijiti mwenzangu, naamini atakuja mtu ambaye ataipeleka
mbali zaidi UDSM."