MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AJITOSA KUWASAIDIA VIJANA WALIOKOSA AJIRA,SOMA HAPO KUJUA
Vijana wametakiwa kuondokana na mawazo ya kuajiriwa
pindi wanapohitimu chuo kikuu bali wametakiwa kubuni nafasi ya kujiajiri au
kubuni biashara mbali mbali jambo litakalowasaidia kuondokana na tatizo la
ukosefu wa ajira,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Hayo yamebainishwa leo na mkuu wa wilaya ya
kinondoni,
Ally Hapi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ujasiliamali kwa vijana zaidi ya 1000 ndani ya Halmashauri hiyo kwa vijana waliohitimu vyuo vikuu na wasiowahitimu vyuo vikuu, kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kubuni biashara na miradi mbalimbali.
Ally Hapi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya ujasiliamali kwa vijana zaidi ya 1000 ndani ya Halmashauri hiyo kwa vijana waliohitimu vyuo vikuu na wasiowahitimu vyuo vikuu, kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kubuni biashara na miradi mbalimbali.
Ambapo Hapi amesema serikali haina uwezo wa kuajiri
wote wanaomaliza vyuo vikuu kutokana na ufinyu wa ajira uliopo jambo
analowataka wahitimi hao kubuni mipango ya kujiajiri.
Amesema kuwa jukumu la serikali ni kuwakea mazingira
mazuri kwa wahitimu hao ili waweze kujiari ndilo jukumu analolifanya yeye
katika kutoa mafunzo kwa vijana ambapo ameleeleza kuwa ameanzisha mafunzo hayo
kwa nia ya kuwaondoa uwoga vijana katika kujiajiri
Kwa upande wake vijana waliopata mafunzo hayo
wamemshukuru mkuu huyo wa wilaya kwa kumuhaidi kutekeleza mafunzo hayo kwa
vitendo