AMANA BENK YAJA NA HILI BORA KWA WATEJA WAKE,SOMA HAPO KUJUA
Diwani wa Kata ya kibonde Maji mbagala Jijini Dar es
salaam Mh Abdala Mtimika (Kushoto) Pamoja na Mkurugenzi wa Bank ya Amana
nchini Dr Mosen Masoud wakikata utepe Kuashiria kuzinduliwa Rasmi kwa Huduma ya
mikopo Midogo Midogo kwa wafanya biashara wa Mbagala Jijini Dar es
salaam.uzinduzi huo umefanyika katika Tawi la Amana Mbagala
|
Hatimaye wakazi wa mbagala wanaofanya Biashara ndogo ndogo wakiwemo wajasiriamali wamepata neema kubwa baada ya Bank ya AMANA kuzinduaa huduma yake mpya ya kutoa mikopo midogo midogo kwa wafanya biashara, huduma ambayo imezinduliwa leo jijini Dar es salaam ikiwa ni miaka mitano Tangu kuanzishwa kwa Bank Hiyo.
Akizungumza na wanahabari na wananchi wa mbagala ambapo ndipo uzinduzi huo umefanyika Mkurugenzi wa Bank Hiyo Dk Muhsin Masoud, amesema kuwa huduma hiyo imeanzishwa mahususi kwa kutambua hitajio kubwa katika jamii la wafanya biashara wadogo wadogo katika kupata mtaji ya kukuza biashara zao hivyo Bank ya Amana imeamua kuwainua wafanya biashara hao wadogo ili kuinuka kipato chao na kufikia kipato cha kati na hata kipato cha juu.
Wiki ya Huduma
kwa wateja ikiendelea wateja mbalimbali wakipata Huduma katika Tawi la Benk
hiyo Mbagala leo
|