Zinazobamba

RC MAKONDA APINGANA NA RAIS MAGUFULI,AIBUKA NA KUAGIZA WAMACHINGA WAONDOLEWE,SOMA HAPO KUJUA

rc-makonda-dc-mo7-1

Kufuatia agizo la Rais John Pombe Magufuli miezi kadhaa iliyopita kutaka kutokubugudhiwa kwa wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama ‘machinga’ na kuachwa waendelee na shughuli zao, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda ameeleza kuwa machinga hao wamekuwa wakienda kinyume na kukiuka tararibu.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam Dar es salaam Makonda ameeleza kuwa machinga wamekuwa wakifanya biashara maeneo yasiyo rasmi ikiwemo maeneo ya barabara za mwendokasi, nje ya hoteli mbalimbali, vituo vya daladala na kuwa kikwazo kwa wapita njia, waendesha Bodaboda na baiskeli.

Akiitaja Kariakoo kama mfano Makonda amesema machinga wamekuwa wakifanya biashara inayofanana na wenye maduka mbele ya maduka yao jambo linalopelekea wao Kukosa wateja, Huku akieleza kuwa uwepo wa Machinga umepelekea kutokukusanywa vyema kwa mapato kutokana na kutokuwa na mfumo maalum ambapo kwa wilaya ya Ilala wamekosa kukusanya bilioni moja ndani ya mwezi Mmoja, halikadhalika suala la usalama na mali za raia umekuwa Mdogo kumekuwepo na matukio mengi ya uhalifu.
Hivyo Mkuu huyo wa Mkoa amewaagiza machinga wote kwenda maeneo waliyopangiwa katika wilaya zao na kutoa siku 14 kwa wakuu wa wilaya kuhakikisha machinga wote wanapelekwa maeneo stahiki.