MICHEZO MICHAFU YA LIPUMBA NA MSAJILI WAKE WA VYAMA ,YAZIDI FICHUKA,MTATIRO ABAINI UOVU HUU,SOMA HAPO KUJUA
Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF) imedai kubaini njama
za Prof. Ibrahim Lipumba waliyemfuta uanachama na kwamba anashikilia kinyume
cha sheria wadhifa wa uenyekiti wa chama hicho, kuwa ana mkakati wa kuchukua
ruzuku ya chama hicho kinyume cha sheria na kuitisha baraza feki ili kufanya
maamuzi ya uvunjaji wa Bodi ya Wadhamini iliyoundwa kihalali na Baraza Kuu la
Uongozi la Taifa CUF.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi
CUF, Julias Mtatiro amedai kuwa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
imemhakikishia Lipumba kwamba, akishafanikiwa kuivunja bodi ya wadhamini ya
chama hicho, Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi atabariki maamuzi
ya baraza hilo aliloliita feki.
Mtatiro amesema baraza lolote
litakaloketi kutokana na wito wa Lipumba waliye mvua uenyekiti, litakuwa si
halali na kufafanua kuwa halitakuwa na akidi halali ya wajumbe kwa kuwa walio
wengi hawamuungi mkono Lipumba hivyo hawatahudhuria.
Ameeleza kuwa, Baraza halali
linalotambulika kisheria na kwa mujibu wa katiba ya chama hicho, ni lile
lililochaguliwa mwaka 2014 ambalo litamaliza muda wake 2019 ambapo amesema kuwa
halimtambui Lipumba kama mwenyekiti wake.
Amesisitiza kuwa, baraza halali
linatakiwa liwe na wajumbe halali 53 na hii ni kutokana na baadhi ya wajumbe
wake 6 kuvuliwa uanachama huku nafasi nyengine 4 zikiachwa wazi na kwamba idadi
kamili ya wajumbe wa baraza hilo inatakiwa kuwa 63.
Kutokana na hoja hiyo, Lipumba
hatokuwa na mamlaka ya kuitisha baraza halali kwa kuwa wajumbe 43 kati ya 53
waliohudhuria katika kikao waliliridhia Lipumba kuondolewa katika chama hicho.
“Chama chetu kinapata taarifa
ya kila kitu kinachoendelea, tuna taarifa mpya kuwa Lipumba amekaa kikao na
Jaji Mutungi katika kuendeleza mikakati ya kuivunja CUF, awali alikwenda Sakaya
katika Ofisi ya Msajili kutafuta namna ya kupata ruzuku ya chama na kwamba wana
wasiwasi kuwa ruzuku ikiingia itachukuliwa na wengine, ” amesema.
Mtatiro amedai kuwa Lipumba amepewa
maelekezo kutoka kwa ofisi ya msajili wa vyama vya siasa ya kutengeneza
utaratibu wa kuvunja kurugenzi za CUF na kwamba baada ya kufanikisha hilo,
atafute wakurugenzi wapya aliowadai kuwa ni feki.
“Lipumba hawezi itisha Bodi
halali ya Wadhamini ikasikia wito wake na kutekeleza maagizo yake sababu hana
mamlaka, jana aliita watendaji wa Baraza Kuu la Uongozi Taifa lakini kwa sababu
hana wajumbe halali walioitikia wito ni hawazidi 6, ila leo hii kamati yangu
ikiita watendaji wanakuja wote hata iwe saa nane usiku, ” amesema.
Aidha, Mtatiro ametoa onyo kwa
Jaji Mutungi kutoendelea kujihusisha na mgogoro wa chama hicho na kumtaka
kutomdanganya Lipumba kuwa ana uhali wa kuendelea kuwa mwenyekiti kwa kuwa
hatambuliki kisheria.
“Msajili hawezi akaamua mambo ya
CUF, hiki ni chama kinaendeshwa kisheria, na wala uamuzi wake siyo wa mwisho
unaweza pingwa mahakamani,” amesema.
Licha ya tuhuma hizo kwa jaji
Mutungi, wabunge wa CUF wameomba kuonana nae na kwamba wanataraji kupeleka
barua rasmi katika ofisi yake ili kufanya nae mazungumzo kwa ajili ya kutaka
kumshauri kutoruhusu ofisi yake kukihujumu chama hicho.
Akizungumza kwa niaba ya
wabunge wa CUF, Riziki Ngwale amesema wabunge wa cuf wataendelea kumsihi jaji
Mutungi kutoingilia mgogoro wa chama hicho unaoendelea sasa.
“Tuanendelea kumsihi jaji
Mutungi kuacha kuhujumu demokrasia kwa kumtambua mtu ambaye chama chetu
hakimtambui. Na sisi wabunge tunaomba kuonana nae kwa ajili ya mazungumzo
naamini atatuelewa,” amesema.