Zinazobamba

WAHAMIHAJI HARAMU 102 WADAKWA DAR,WENGI NI WACHEZA MUZIKI,SOMA HAPO KUJUA


Afisa Uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam, Naibu Kamishna, Johannes Msumule akizungumza katika mkutano na Waandishi wa Habari.
Pichani ni Kamishna wa Idara ya Uhamiaji mkoani Dar es Salaam, John Msumule picha na Maktaba




NA KAROLI VINSENT
IDARA ya Uhamiaji mkoani Dar es Salaam imewamata wahamiaji haramu 102 ambao wameingia nchini pasipo kiharali.

Hata hivyo,pia idara hiyo imewakamata Watanzania watatu ambao walihusika katika kuwahifadhi wamiaji hao pamoja na kuwazuia maafisa uhamiaji kutotimiza majukumu yake.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini hapa,Kamishna wa Idara ya Uhamiaji mkoani Dar es Salaam, John Msumule ambapo amesema wahamiaji wamekamatwa baada ya idara hiyo kufanya msako mkali ambao ulianza tangu mwanzoni mwa mwezi na kufanikiwa kuwakamata wahamiajia hao.

Amesema wahamiaji ambao wengi wao wametoka nchi za India pamoja na Nepal  walikamatwa kwenye  Kampuni moja iliyopo  Mikocheni wilaya ya Kinondoni Jijini hapa  ambapo amedai baada ya kuwakamata na kuwahoji walibainika wamekuja hapa kwa shughuli za kucheza mziki.

Amesema mara baada ya maofisa wa Uhamiaji kuwataka waonyeshe kibari cha kuingia nchini ambapo wahamiaji hao walionyesha kubari ambacho mda wake wa kuishi nchini ulikuwa umekwisha huku wao wakiendelea kuishi bila ya kutoa taarifa kwenye Idara hiyo.

Hata hivyo,Kamishna Msumule amesema pia Idara yake inawashikilia watanzania watatu ambao walihusika katika kuwahifadhi wamiaji hao kwa lengo la kuwaficha watu hao ili mamlaka usika zishindwe kuwakamata pamoja na kuwatafutia nyaraka zitakazowawezesha kuishi nchini.

Vilevile,amesema Wahamiaji hao pamoja na watanzania hao,watafikishwa Mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.
Sanjari na hayo,,Kamishna Msumule amesema Idara yake inakumbana na changamoto ambazo amedai zinachangia kushindwa kufanya kazi kikamilifu za kupambana na wahamiaji hao.
Amezitaja Changomoto hizo,Ukosefu wa Magari amabyo watayatumia kufanya Doria,pamoja uhaba wa Rasirimali watu,hivyo ameiomba Serikali kutatua changomoto hizo ili Idara hiyo iweze kupambana na wahamiajia haramu.

Hakuna maoni