MRITHI WA PAUL MAKONDA KINONDONI AJA NA KASI YAKE,AWAJIA JUU WAKAZI WA KAWE,SOMA HAPO KUJUA
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Salum akizungumza na Mmiliki wa Nyumba ambaye nyumba yake ni miongoni mwa Nyumba zilichini ya Udongo,ambapo Nyumba yake mkazi huyo ipo katika eneo hatarishi
Pichani aliyevaa koti ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Salum atia amri kwa watendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wananchi wa Kawe kwa Mkwamani ambao wanaishia katika maeneo hatarishi wawe wamehama ndani ya saa saba,
Sehemu ya Udongo huo,ambao mda wowote unaweza kushuka kwenye Nyumba za nchini
Pichani aliyevaa koti ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Salum atia amri kwa watendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wananchi wa Kawe kwa Mkwamani ambao wanaishia katika maeneo hatarishi wawe wamehama ndani ya saa saba,
Sehemu ya Udongo huo,ambao mda wowote unaweza kushuka kwenye Nyumba za nchini
sehemu ya Nyumba ambazo kati ya 30 ambazo wakazi wake wameamriwa kuhama kabla ya saa mbili usiku wa leo
NA KAROLI VINSENT
MKUU wa Wilaya Kinondoni,Salum Happi amewapa mda wa
saa saba, yaani mpaka saa mbili usiku wa leo, nyumba 30 za wakazi wa Kawe mtaa
wa Ukwamani wawe wameondoka mara
moja katika eneo hilo kutokana na kuishi eneo hatarishi.
Mkuu huyo wa
Wilaya ambaye ameapishwa juzi Alhamisi na Rais John Magufuli mara baada ya kuchukua nafasi hiyo iliachwa wazi na
Paul Makonda ambaye sasa ni Mkuu wa mkoa
wa Dar es Salaam,
Wakazi hao ambao wanaishi katika Bonde ambalo juu ya nyumba hizo kuna udongo pamoja Nyufa za nyumba ambazo wakati wowote zinaweza kuanguka na kuleta
madhara kwa wananchi hao kwa nyumba zao kufukiwa na udongo huo kutokana mvua
zinazoendelea kunyesha.
Happi, ametoa agizo hilo mda huu ,mara baada ya
kufanya ziara kwenye maeneo hayo ambapo,amesema yeye kama kiongozi wa Ulinzi wa
Usalama katika Wilaya hiyo hatakubali kuona wananchi wake wanakufa kutokana na mafuriko.
Happi,amewataka watendaji wote wa Halmashauri ya
Kinondoni wakiongozwa na Katibu Tawala wa Wilaya kuhakikisha wakazi hao wanaondoka
kabla ya kufika saa mbili usiku,
Huku pia akitoa wazo wa wakazi hao kutafutiwa maeneo
ya kuhifadhiwa kwenye eneo la shule
mpaka pale watakapopata eneo zuri la kuishi.
Kwa Upande wao Wakazi hao wa ambao wameamliwa kuhama
walimweleza mkuu huyo wa Wilaya kuwa,hata wao wanatamani kuondoka maeneo hayo
kutokana na kufahamu wanaishi eneo hatarishi ila jambo linawazuia ni hawajui
wapi watakwenda kushi kutokana na maisha magumu wananayoishi.
Majibu hayo,yalimfanya mkuu huyo Wilaya kuwasihi
watafute hata maeneo yoyote ya kuishi ili kuokoa maisha yao ambayo amedai yapo
katika hatari kubwa sana.
wanawaondoa
waka
Hakuna maoni
Chapisha Maoni