MEYA ILALA AFUATA NYAYO ZA RAIS MAGUFULI
Imeelezwa kuwa kutumbua majipu
hakuchagui dini, rangi wala kabila, au itikadi yeyote ile bali kunatokana na usimamizi mbovu wa sheria au kutofuata sheria za nchi katika utumisjhi wa umma.
Hayo yameonekana baada ya Mstahiki Meya wa Ilala Charles
Kuyeko kuwatumbua watumishi watatu wa manispaa hiyo kwa kutokana na usimamizi
mbovu wa miradi ya barabara za wilaya hiyo.
Akizungumza jijini Dar
es Salaam leo Mstahiki Meya Kuyeko amesema wilaya yake imejipanga kusimamia miradi
ya maendeleo katika wilaya hiyo ina wanufaisha wanachi wote hivyo kutokana na
kikao kilichofanywa na madiwani mwishoni wa wiki wameadhimia kumsimamisha kazi
Mhandisi mkuu Japheri Mwigane na watumishi wengine ambao ni Siajari Mahili na
Daniel Kiligiti.
Meya amesema watumishi
hao wamekuwa wakilalamikiwa kwa muda mrefu na madiwani wa wilaya hiyo lakini
wamekuwa hawayafanyii kazi malalamiko hayo jambo ambalo limemplelekea meya
kuchukua hatua hiyo ya kuwasimamisha kazi kutokana na usmamizi mbovu wa
barabara, akiitolea mfano wa barabara ya Moshi Bar.
Katika hatua nyingine
Mstahiki Meya Kuyeko ameeleza kuwa Manispaa yake imetenga bilioni 85 kusimamia
miradi ya maendeleo tofauti na bajeti za miaka iliyo pita hivyo anaimani
kutokana na bajeti hiyo itaweza kutatu suala la miundombinu, huduma za Afya,
suala la elimu kwa kuongeza vyumba vya madarasa na madawati ambapo wameishaanza
kujenga madarasa kuanzia matano mpaka nane kwa shule zenye upungufu.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni