WIZARA YA MAGUFULI KUITIA HASARA SERIKALI BILIONI 124.8,PPRA WASEMA HASARA HIYO KUONGEZEKA,SOMA HAPO KUJUA
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvubFVFDW-_YOr96dpN6gdLuutyelIP1ov_Sri3jXOEvcwbe19f9pNkGCcfIk8KYDVKiaAg4Y_egPzngVpLOgPxnLWlk1LLYf93spoTC7gMtIZG8yragnTHcwgzKE2bdRc2Px_YgzBpZg/s1600/1.jpg)
WIZARA ya Ujenzi imetajwa kuitia hasara serikali ya
Tanzania jumla ya Bilioni 124.8 kutokana
na kuchelewesha kulipa deni la trilioni 5.3 kwa makandarasi.Anaandika KAROLI
VINSENT endelea nayo.
Hayo
yamesema leo jijini Dar es Salaam na Afisa Mtendaji mkuu wa Tume ya manunuzi ya
Umma (PPRA) Dk Shirima wakati wa mkutano
na waandishi wa habari ambapo amesema
tume hiyo imebaini hasara hiyo baada ya kufanya ukaguzi kwenye Wizara hiyo ambayo inayongozwa na
Mgombea Urais wa Chama cha Mapinduzi CCM Dokta John Magufuli
Na
kukuta ucheleweshaji mkubwa wa kulipa deni
makandarasi husasani kwenye miradi ya ujenzi wa barabara ya ujenzi wa barabara nchini ya TANROADS na miradi ya maji kwenye serikali za mtaa.
Dk
Shirima amebaisha kuwa jumla ya mikataba 301 ya TANROADS yenye thamani ya
trillion 5.3 ilicheleweshwa malipo na hivyo kuwa na malimbikizo ya riba ya
shilingi Bilioni 124.8 hadi mwezi
juni.2015.
Hata
hivyo Dk Shirima amesema riba hiyo itazidi kuongezeka hadi hapo malipo
yatakapofanyika.
Sanjari na hayo,PPRA imezitaja taasisi
9 ambazo zimekuwa na viashiria vya rushwa ya kutisha katika utendaji
wake ikiwemo katika kufanya manunizi.
Amezitaja taasisi hizo ni Tume ya Taifa ya uchaguzi
nchini,Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni,Halmashauri ya wilaya ya
Mpanda,Kampuni ya reli nchini TRL,Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo,Halmashauri
ya wilaya ya kigoma,Halmashauri ya Wilaya Mbozi pamoja na Halmashauri ya Wilaya
ya Karatu.
Katika Hatua nyingine PPRA imezifungia miaka miwili kampuni
6 pamoja na kufingia kampuni moja kwa kipndi cha Miaka 10 baada ya kubainika
walifanya udanganyifu ikiwemo kufoji ili kupata tenda ya dhabuni.
Kampuni sita hizo ni
M/s Intersysten Holding Company ,limited,M/s PEMA TECH Company
Limite,M/S Nyakatire Investment Limetd.
Kampuni nyengine ni Kosemwa Propsects Company Limetd
,Ms Perntels Company Limited,MS Car and
general Trading Limited.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni