Zinazobamba

TAARIFA KUHUSU JENERAL MWAMUNYANGE KUWEKEWA SUMU.UKWELI WAKE HUU HAPA,SOMA HAPO KUJUA


NA KAROLI VINSENT
WAKATI kukiwa kuna taarifa zinazoenezwa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii zikisema mkuu wa Majeshi  ya ulinzi  nchini Jeneral Davis Mwamunyange kuwa  amewekewa sumu na hali yake sahivi kuwa mbaya,,
          Huku,taarifa hiyo ikisema sababu ya kuwekewa  sumu huko, imetokana na masuala ya kisiasa,hatimaye Serikali imeibuka na kukanusha taarifa hizo na kusema ni za uongo zenye nia ya kufakaranisha Taifa.
      Akikanusha Uvumi huo, leo Jijini Dar es Salaam  wakati wa mkutano na waandishi wa habari, Afisa Habari wa Serikali ambaye pia ni mkurugenzi wa Idara ya Habari –Maelezo Assah Mwambene amesema Jeneral Mwamunyange yupo salama na anaendelea na kazi zake,akidai kuwa taarifa hizo zinalengo  ya kuchonginisha watanzania na jeshi na kuharibu picha ya Amani na utulivu uliopo nchini.

Pichani ni Mkurugenzi wa Idara ya habari Maelezo Asssah Mwambene akizungumzana waandishi wa habari
  
         Mwambene amewataka Watanzania kupuuza taarifa hizo huku akiwasihi kutoingiza siasa kwenye masuala nyeti ya nchi ikiwemo jeshi,kwani jeshi ni taasisi isiyojihusiha na siasa.
     Wakati huo huo pia Serikali imetolewa ufafanuzi juu ya taarifa  zilizoandikwa kwenye Gazeti la Tanzania Daima  ambazo zilikuwa zinaubeza  uteuzi uliofanywa hivi karibuni na Rais Jakaya Kikwete kwa kuwateua wakuu wa wilaya wapya, wakidai uteuzi huo ulikuwa ni   wakulipa fadhira kwa kwa wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM.
     Akifafanua uteuzi huo,Mwambene amesema watu wanaobeza ni uteuzi huo watakuwa hawajui sheria za nchi na kufahamu mamlaka ya Rais,
Amesema kwa mujibu wa sheria.kanuni za nchi  na taratibu  Rais anamamlaka  ya kufanya uteuzi  wakati wewote inapobidi kwa malengo ya kuboresha utendaji wa kazi  serikalini.
“Serikali imesikitishwa na taarifa zilizotolewa na gazeti la Tanzania daima kuhusiana na uteuzi  wa Rais,taarifa hizi ni za kichochezi na zinalenga kumchonganisha Rais na wananchi wake”amesema Mwambene.
    Aidha,Mwambene amevitaka vyombo vya habari nchi kufanya utafiti na kusoma kabla ya kuandika habari ,na pia  akavihasa kuandika habari zenye lengo la kujenga umoja na mshikamo badala ya kuandika habari zenye lengo kuwagawa Watanzania 

Hakuna maoni