UTATA WAIBUKA GAZETI LA MTANZANIA KUTOONEKANA MTAAN LEOI,MHARIRI WAKE ANG'AKA,SOMA HAPO KUJUA
UTATA mzito umeibuka kuhusu kutoibuka leo mtaani
Gazeti linalotoka kila siku la Mtanzania.(Mtandao huu umedokezwa).Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo.
Maswali
mengi yaibuka mtaani husasani kwa wauza magazeti pamoja na wasomaji ambao wengi
walikuwa wananufaika na Gazeti hilo pendwa kwa sasa hapa nchini na wamekuwa na
maswali mengi kutonekana leo.
Kwa
mujibu wa mtoa taarifa wa Fullhabari.blog aliyoko ndani ya ofisi la Gazeti la
Mtanzania ameuambia mtandao huu kuwa gazeti hilo halijatoka mtaani kwasababu ilichapisha
habari moja kubwa ambayo ilyoonyesha ubadilifu mkubwa wa fedha za umma ndani ya Serikali ambayo yalibuliwa na Mamlaka
ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) kwa mwaka wa fedha 2014/15
Chanzo chetu hicho kimezidi sema kuwa Gazeti hilo
lilitoka ila inadaiwa nakala zake zote
zilinnuliwa zote ili zisifike kwa wananchi bila hata kumtaja aliyenunua nakala hizo,ambapo ndio maana Gazeti hilo
alijatoka kabisa siku ya leo ya tarehe 7-10-2015,
Huku Gazeti hilo likionekana mtandaoni likiweka habari hiyo kama unavyoona mchoro ambapo ilitakiwa iwe kwenye ukrasa wa mbele
Huku Gazeti hilo likionekana mtandaoni likiweka habari hiyo kama unavyoona mchoro ambapo ilitakiwa iwe kwenye ukrasa wa mbele
WAUZA MAGAZETI WAFUNGUKA
Katika kuthibitisha madai hayo mtandao huu ulijalibu
kuongea na wauza magazeti katika mkoa wa Dar es Salaam kutaka kujua je kwa siku
ya leo wamepata nakala za Gazeti hilo,
Joseph Elias ambaye anauza magazeti maeneo ya Posta
jijini hapa amesema hata wao wanashangaa kwanini leo gazeti la Mtanzania
alijafika kwa mawakala ambao wanawapa magazeti ili wayauze.
“Ujue
mimi mwenyewe nimeshangaa huwaga haijawi kutokea Gazeti hili kutofika mtaani
labda liwe limefungiwa lakini hili alijafungiwa kwahiyo tumeshangaa sana,yaani
biashara zetu leo ziko vibaya,kwani gazeti hili linatuingizia pesa sana’amesema
MHARIRI WA MTANZANIA ANENA
Fullhabari.blog ilijalibu kumtafuta mhariri wa Gazeti
hilo Aradia Peter, kutaka kujua juu ya taarifa hizo, ambapo naye alishangaa
mwandishi wa habari hizi amezipata wapi taarifa hizo ambapo ndipo akasema
Gazeti la Mtanzania alijatoka leo barabarani kwasababu ya mtambo wa kuchapishia
Gazeti hilo kuharibika dakika za mwisho,
“Hizo taarifa ni za uongo kwani Gazeti la Mtanzania
alijatoka leo kwasababu ya mashine zetu za kuchapishia kupata itilafu kidogo
ndio maana alijatoka”
Mwandishi wa Fullhabari.blog amkambana juu ya majibu
yake hayo kwamba,kama mashine zilikuwa
na itilafu mbona Gazeti la michezo la Dimba ambalo nalo linatumia mitambo hiyo
limechapishwa na liko mtaani?akajibu kwa kusema
“Mbona kama ndio hivyo Gazeti limetoka maeneo ya
Kanda ya ziwa ambapo kuna mashine zengine”
Hakuna maoni
Chapisha Maoni