Zinazobamba

WAZIRI LUKUVI AKUBALI KUWEPO WEZI WIZARANI KWAKE,NI WALE WANAOWAHUJUMU WANANCHI,SOMA HAPA KUJUA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi. Picha: Mwananchi

WAZIRI wa Ardhi,nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi(pichani) amekili wizara yake imegubikwa na rushwa kubwa kwa Watendaji wa Ardhi Jambao ambalo anasema limeleta uhasama kwa wananchi na kuzidisha migogoro ya Ardhi nchini.Anaandika KAROLI VINSENT,endelea nayo
          Waziri Lukuvi amesema hayo leo wakati wa Mkutano uliowakutani watumishi wa Sekta Ardhi katika mkoa wa Dar es Salaam wenye lengo la kuwapa uwezo ili wafanye kazi bila kuwepo kwa kero kwa wananchi ambapo Waziri lukuvi amesema kwa sasa hali ya migorogoro ya Ardhi ndani ya mkoa wa Dar es Salaam imekuwa kubwa sana inaimesababishwa  na utendaji  mbovu jambo ambalo anasema limewafanya wananchi wakose na Imani na Serikali.
                Waziri Lukuvi ameongeza kuwa hata jambo la kuchelewesha kutolewa kwa hati za Viwanja kwa Wananchi limesabishwa na watendaji hao kuzidisha Urasimu wa kutoa Rushwa kwani amesema kwasasa wananchi wamekuwa wakisota kwenye Halmashauri mbalimbali kutaka kupata hati ya viwanja kwa mda wa miaka 15.
         Amebainisha kuwa Suala la Hati ya viwanja kisheria linatakiwa kumalizwa ndani ya miezi sita na Mwananchi kukabidhiwa hati yake,lakini kutokana na Utendaji Mbovu wa watendaji umechangia hati hizo kucheleweshwa kwa wananchi.
              Aidha, Waziri Lukuvi amesema kama kiongozi safi hato kubali kuona urasimu na akawataka watendaji ndani ya siku 20 wawe wametatua tatizo la mgogoro wa Ardhi.

          Vilevile Waziri Lukuvi Akawataka Wananchi kutosita kutoa taarifa kwenye Viongozi husika kwenye Wizara hiyo ili hatua zishukue kwa Watendaji ambao anasema ni kikwazo kwenye wizara yake

No comments