HABARI KUBWA LEO-MBOWE AUMBULIWA NA NEC,KAULI YAKE YASUTWA,SOMA HAPA KUJUA
TUME ya uchaguzi nchini (NEC)imesema tarehe ya
Uchaguzi mkuu Mwaka huu,ipo pale pale siku ya terehe 25 mwezi octoba mwaka huu.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Kauli ya NEC inakuja ikiwa siku moja kupita
baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Freeman Mbowe
kuitangazi serikali kiama endapo itasogeza mbele tarehe ya uchaguzi mkuu kwa –
Madai ya tume hiyo kushindwa kuwaandikisha wananchi kwa
wakati kwenye Daftrari la wapiga kura kwa mfumo mpya wa Biometric Vote
Regislation BVR.
Akifanunua Kauli hiyo ya Mbowe mda huu Jijini Dar es Salaam naMwenyekiti wa NEC Jaji mstaafu Damian Lubuva wakati wa Mkutano na Waandishi wa
Habari ambapo amesema taarifa zinazosemwa na wanasiasa kwamba tume hiyo
itasogeza mbele uchaguzi Mkuu si za
kweli zinalengo la kuwachanganya wananchi,kwani tume hiyo inakwenda vizuri na
uandikishaji wa Mfumo mpya wa BVR.
Jaji Damian ameongeza kuwa kwa sasa
Uandikishaji wa Wapiga kura kwenye Mkoa wa mdogo wa Njombe wanatarajia kumaliza
kesho na kuanza rasmi uandikishaji kwenye mikoa mingine ya Mtwala.lindi na
Iringa ambapo anasema kwa sasa watafanya kwa kasi zaidi.
Amebainisha kuwa tatizo la lilokuwa
linawakabili kwa kuwa na mashine chache za uandikishaji wameliweza kulitatua
kwakuwa sahivi tayari mashine zengine 1600 zinatarajiwa kuwasili siku ya kesho
na kuongeza idadi ya mashine za sasa 250 jambo ambalo anadai litafanikishwa
kasi ya uandikishaji.
Aidha,Amesema shehena nyingine ya
mashine itarajiwa kuja tarehe 25 mwezi huu na mpaka ifikapo mwezi wa Sita mwaka
huu watakuwa wameshapata mashine zote elfu nane walizokuwa wakiziitaji jambo
ambalo anazidi dai litawafanya wamalize kuwaandisha wananchi nchi nzima kwenye
mwezi wa saba mwaka huu.
Vilevile
Jaji Damian akawataka wanasiasa kuwacha kuwapotosha wananchi kuhusu
uandikishaji huo jambo ambalo anasema linaweza kuleta machafuko nchini.
No comments
Post a Comment