BREAKING NEWS-NYUMBA YA ASKOFU GWAJIMA YAZINGILWA KUNDI LA POLISI SOMA HAPA KUJUA
HABARI
zilizotufikia mda huu zinasema nyumba ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima
Josepht Gwajima (pichani) imezingilwa na kundi la Polisi, kwaanzia Majira ya saa moja asubuhi
ya leo, huku Askofu huyo akijifungia ndani ya nyumba yake akikataa kufungua
mlango.
Kwa mujibu wa Mwandishi wa Mtandao huu
KAROLI VINSENT aliyoko Nyumbani kwake Askofu Maeno ya Tegeta Jijini Dar es
Salaam zinasema Zaidi ya magari manne ya Polisi aina ya Difenda zimezingila
nyumba hiyo wakiwa na lengo la kumsubili kiongozi huyo wa kiroho atoke ili
wamtia nguvuni pamoja na kufanya msako kwenye nyumba yake.
Mtandao huu
ulimtafuta Kamanda kanda Maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova kutaka kujua
kurikoni wamenda gafla kwenye nyumba ya Askofu huyo haya ndio majjibu yake
aliyomjibu Mwandishi wetu.
“Acheni mambo yenu ya kiundishi wa Habari hapa nipo kwenye Kikao muhimu sana hayo ya
Askofu Gwajima nitawajibu baadae”amesema Kamishna Kova
ENDELEA
KUFUATILIA MTANDAO HUU UTAPATA TAARIFA KAMILI BAADAE
No comments
Post a Comment