Zinazobamba

TGP WAMUANGUKIA RAIS KIKWETE,NI KUHUSU MSWAADA WA MTANDAONI SOMA HAPA KUJUA

pichani ni Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano wa TGP
Bwana Temba Akitoa semina ya mafunzo kwa waaandishi na

Wamiliki wa Blogs mbalimbali

WADAU mbali mbali wameendelea kumlilia Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Rais Jakaya Kikwete asisaini Maswaada wa sheria ya uharifu Mitandaoni wa mwaka 2015 kwa kusema mswaada huo  unavingere ambayo wanasema vitauzikia Uhuru wa Habari nchini na pamoja na uhuru wa  kutoa maoni kwa wananchi.Anaandika KAROLI VINSENT.Endelea nayo
            Hayo yamesemwa Leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa  Mtandao wa Jinsia nchini (TGP) Lilian Liundi wakati wa Semina iliyowakutanisha waandishi mbalimbali na wamiliki wa Mitandao ya Kijamii yenye lengo la kuwajengea uwezo wa kuripoti taarifa mbalimbali hususani katika kipindi hiki muhimu cha kura ya Maoni ya kupitisha katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la katiba pamoja na Uchaguzi Mkuu hapo baadae Mwaka huu.
Waaandishi Mbali mbali wa Mitandaoni wakiwa kwenye makini wakisikiliza mafunzo yanayotolewa na
 Watendaji wa TGNP

          Ambapo Bi Liundi amesema licha ya mswaada huo kuwa na vipengere vya kuzuia uharifu wa watu wanaofanya makosa mitandaoni lakini umekuwa na vipengere ambavyo anasema ndio  vitakuwa vimeua Uhuru wa Habari nchini
       Bi Liundi ametolea mfano kipengere cha sheria kilichokuwepo kwenye mswaada huo ambacho kinamtia hatiani mtu anayetuma picha ya matusi na vilevile kinamtia hatiani mtu anayepokea picha hiyo kwa kusema kipingere hicho kinautata na kitawafanya watanzania wengi kuingia hatiani.
          Pamoja na hayo amebainisha kuwa kwa sasa TGP wameshatoa matamko ya kumtaka Rais Kikwete asiweke sahini kwenye mswaada huo.
         Kwa upande wao Wamiliki pamoja na waandeshaji mbali mbali ya Mitandao ya Kijamii nao wameendelea kumuomba Rais Kikwete pia asiweke saini kwenye Maswaada huo wa Mwaka 2015 miongoni mwao ni Evanc Bukuku ambaye ni Mmiliki wa Mtandao wa “Fullshangwe.Blogs”amesema anaamini Rais Kikwete ni Mtu sikivu jambo ambalo anadai atasikia kilio cha watanzania pamoja na wadau mbali mbali kutoweka saini kwenye mswaada huo.
    Mbali na Bukuku mwengine ni Selemain Magari ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa Fullhabari.blogs naye pia amemtaka Rais kikwete kutia saini mswaada kwa kusema utaliweka Taifa njia panda





No comments