KUBWA-TANESCO KUZIMA MITAMBO YAKE,NI ILE YA AGREKO,IPTL,KILIO CHA ZITTO KABWE CHATIMIA,SOMA HAPO KUJUA
| sehemu ya Mitambo ya Kinyerezi iliyotembelewa na wanahabari leo |
SHIRIKA la
umeme nchini (TANESCO) liko mbioni kuizima mitambo yake ambayo inatumia mafuta
mazito katika kuzalisha umeme, baada ya kukamilika kwa asilimia 84 mitambo yake mipya na ya kisisasa inayotumia
Gesi iliyoko Tabata kinyerezi Jijini Dar es Salaam.Anaripoti KAROLI
VINSENT,Endelea nayo
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es
Salaam na Meneja miradi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) Mhandisi Simon Jilima
wakati wa ziara na Waandishi wa Habari kwenye mitambo mbali
mbali ya shirika hilo ambapo Mhandisi Jilima amesema mitambo ya kinyerezi
imekamilika kwa asilimia 84 na inatarajia kukamilika kabisa hapo mwanzoni mwa mwezi wa sita mwaka huu,ambapo-
Anadai kukamilika kwa mitambo hiyo
kutalisaidia shirika hilo kuachana na mitambo ambayo inatumia mafuta mazito
ambapo anasema mitambo hiyo imekuwa mzigo kwa Tanesco kutokana na kupata hasara kubwa za kununua mafuta za kuendesha mitambo hiyo.
Mhandisi Jilima alibainisha kuwa
kukamilika kwa mitambo ya kinyerezi
itapelekea kupatikana kwa megawati 150 ambazo zitakwenda moja kwa moja
kwenye Gridi ya Taifa.
Vilevile amesema kukamilika kwa kabisa kwa
mitambo inalifanya shirika hilo kuachana na makambuni ambayo yanaiuzia umeme
shirika hilo ,yanaotumia mitambo ya mafuta.
Aidha Mhandisi Jilima aliitaja mitambo
hiyo inatumia mafuta mazito inayotarajiwa kuzimwa ni ya Agreko na Symbion
pamoja na ya IPTL.
Mtambo huo wa Kinyerezi 1 unaojengwa na kampuni ya
Yakobsen Elektro ya Norway unatarajia kukamilika mapema Juni mwaka huu.
Mbali na mitambo ya Kinyerezi,shirika la umeme
nchini Tanesco pia linakamilisha vituo vyake mbalimbali vya kupoza na kusambaza
umeme.vituo hivyo ambavyo waandishi mbali mbali wa Habari walivishuhudia, vipo
katika hatua ya mwisho,ni kilichopo Gongo la Mboto jijini hapa,Kipawa pamoja na
kilicho katika ya Jijini la Dar es Salaam karibu na mahakama ya Kisutu.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa shirika la umeme nchini Tanesco, Mhandisi Felchesmi Mramba anasema kukamilika kwa vituo hivyo ambapo
vinatarajiwa kukamilika vyote mwishoni mwa mwaka huu anasema itasaidi kumaliza
tatizo la umeme kwa sasa ambalo limetokana na mitambo ya sasa kwenye shirika la
Tanesco kuchoka na kuelemewa uwezo.
“Nataka niwaaambia wananchi wa Dar es
Salaam kwa sasa ifikapo mwishoni mwa mwaka huu,mitambo yote itakuwa imekamilika
kwa asilimia 100,na kukamilika kwake kutasaidi kabisa kumaliza tatizo la
kukatika umeme ambalo limekuwa kero kwa wananchi”amesema Mhandisi Mramba.
Mhandisi Mramba ameongeza kuwa sababu ya
kukatika umeme mara kwa mara ilitokana na mitambo ya shirika hilo kuchoka na
kuwafanya wafanyakazi kuhangaika ila kwa mitambo mipya inayotarajiwa kukamilika
anadai itakuwa ni ya kisasa ambayo inatumia teknolojia ya kisasa ya kumpyuta
ambayo haitaitaji wafanyakazi wengi.
Aidha,Mhandisi Mramba anasema mitambo hiyo ya kisasa ni mizuri,mhandisi huyo
amesema endapo kutatokea tatizo la kukatika kwa umeme sehemu kumpyuta ndio
zitaonyesha na itapelekea kuondoa utaratibu wa sasa ambao unawafanya wananchi kuripoti kwenye shirika hilo endapo umeme
ukikatika.
Kuzimwa mitambo ya umeme inayotumia mafuta mazito,itakuwa imemaliza kiu ya aliyewai kuwa mbunge wa kigoma Kaskazini Zitto Kabwe ambapo alipokuwa mbunge alikuwa anaitaka serikali kuachana na mitambo hiyo kutoka na kutumia pesa nyingi.
No comments
Post a Comment