CHUO KIKUU HURIA CHAZIDI KUKUA,SASA KUANZISHA "COLLEGE"YAKE,PFOFESA MBWETE AZIDI WEKA HISTORIA SOMA HAPA KUJUA
| Pichani ni Profesa Mbwete |
CHUO Kikuu Huria nchini (OUT) kipo katika mchakato wa kufanya maboresho
ya mfumo wa utoaji wa elimu ambapo sasa kitaanzisha vyuo katika ngazi ya mkoa (College).Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Katika mabadiliko hayo
chuo hicho pia kitafungua matawi katika ngazi ya wilaya kwa kushirikiana na Halmashauri ya za wilaya.
Makamu Mkuu wa OUT
Profesa Tolly Mbwete ameeleza hayo leo alipokuwa akiongea na wana jumuiya ya chuo
hicho katika mkoa wa Temeke ambao wamemuandalia sherehe ya kumuaga, kufuatia
kuteuliwa kwake kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vyuo vikuu barani Afrika.
Amesema mchakato
wa mabadiliko hayo tayari umepata Baraka za Tume ya Vyuo Vikuu nchini na kwamba
muda si mrefu OUT itaanzisha college katika ngazi ya mikoa.
Kwa upande wake
Mkurugenzi wa OUT mkoa wa Temeke Dk. Jacquiline Bundala amesema tangu
kuanzishwa kwa kituo hicho mwaka 2007 chuo hicho kimepata mafanikio makubwa.
Ameyataja baadhi ya
mafanikio hayo ni pamoja na kuongeza idadi ya wanafunzi kutoka wanafunzi 258
waliokuwepo wakati huo hadi zaidi ya 600 waliopo sasa.
Pamoja na mafanikio hayo Dk. Bundala pia amesema chuo hicho mkoa wa
Temeke kinakabiliwa na tatizo la mtandao ambao ni nyenzo muhimu kwa ajili ya
kujifunza.
Kwa upande wake Rais wa
Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria mkoa wa Temeke Malimi Ntegwa ameutaka
uongozi wa chuo hicho kutatua changamoto zinazowakabili wanafunzi ikiwemo
tatizo la upatikanaji wa vitambulisho, sehemu za kujifunzia hasa wakati wa
vipindi vya ana kwa ana.
mwisho
No comments
Post a Comment