Zinazobamba

WAZIRI NYALANDU ATANGAZA KIAMA NA MAJANGILI,SASA KUTUMIA WANAJESHI KUTOKA UJERUMANI,SOMA HAPA KUJUA


WAZIRI wa Maliasili na Utalii (pichani) Waziri Lazaro Nyalandu amewatangazia Majangili wa wanyama wa tembo popote walipo kuachana na kazi hiyo, kutokana na Mikakati mizito aliyoipanga ikiwemo ya Ulinzi ambao atashirikiana na wanajeshi kutoka nchini Ujerumani,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
     Waziri Nyalandu ametangaza kiama hicho leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambao ulikuwa na lengo la kuzungumzia siku ya wanyama pori duniani,ambapo amesema kwa sasa haoni sababu ya kuendelea kuwaachia majangili kuua wanyama wetu husani Tembo.
         “Kwa sasa nawapa salamu majangili popote walipo nchini,kwamba tumejipanga nawahakikishia ni kwamba watafute kazi ya kufanya,tumejipanga,maana hautuwezi tukawaachia watu wachache wamalize wanyama wetu ambao ni hazina kubwa sana nchini na duniani”amesema Waziri Nyalandu.
        Waziri Nyalandu ameongeza kuwa kwa sasa wameamua kushirikiana na Wanajeshi kutoka nchi za ulaya kuja kuwafundisha ujuzi Askari wa wanyama pori, ujuzi wa kivita ili waweze kupambana na Majangili.
           Alibainisha kuwa haona haja ya watanzania kuwavumilia watu wa aina ya majangili ambao wanataka kuharibu neema ya kipekee ya nchi yetu.
          “Leo Tanzania ni nchi ya pili kuwa na wanyama pori wengi sana ukitoa nchi ya Brazili,na pia Tanzania ni nchi ya pili barani Afrika kuwa  na tembo wengi sana,sasa neema hii yote hii tuwaachia majangili waifute nasema haitowezekana na lazima tuwamalize”Amebainisha Waziri  Nyalandu.

         Aidha, Waziri Nyalandu amewataka watanzania kushirikiana na Askari wa wanyama pori kupambana na Majangili popote walipo.

Hakuna maoni