UKAWA YALIPULIWA HADHARANI, CHAMA ADC CHACHAMAA SOMA HAPA
Chama cha ADC kimechukua maamuzi magumu ambayo yameshindwa na vyama vya upinzani vingine kikiwamo chama cha mapinduzi, na umoja wa kutetea katiba maarufu kwa jina la ukawa baada ya kuamua wanachama wake kujikita dhaidi katika kusoma katiba inayopendekezwa ili siku ya kupiga kura waweze kuwa katika mazingira mazuri ya kuamua,
Akizungumza katika siku ya kuzindua Umoja wa wanawake wanaunda chama hicho, pamoja na umoja wa vijana wa chama hicho mapema hii leo, Mwenyekiti wa Chama hicho Tiaifa, Bw. Saidi Miraji, amesema Wamefikia hatua hiyo baada ya kubaini kuwa kuna haja ya wanachama wao kusoma katiba inayopendekezwa ndipo hapo wanatakuwa na uwezo wa kujua ni kitu gani kipo katika katiba na kama inawafaa wapigie kura ya ndiyo na kama wanaona itakuwa ni janga kwa taifa basi wapige kuya ya hapana,
Amesema Msingi wa kuruhusu watu wwasome katiba unajengeka katika maana ya kumpa mtu uhuru wa kuamua, huwezi wewe mtu mmoja unasoma katiba kisha unasema katiba haifa, huu ni ukiritimba na siasa ambazo si shirikishi ni vyema watu wakaachiwa kuamua wenyewe,
Aidha mkuu huyo wa chama ameendelea kusema kuwa, chama chake kitahakikisha kinasambaza katiba inayopendekezwa hadi vijijini kwa wanachama wake ili wapate fursa ya kuisoma na kutoa maamuzii,
Ndg Zangu nataka niwaambie kuw kukaa kimya na kususia mchakato si dawa, Kwa vyovyote vile katiba hii inayopendekeza itapigiwa kura, na maccm sasa ili tuweze kupambana nao lazima na sisi tusome katiba na tukaamue kwa kupitia kura, kura ndiyo silaha yetu aliongeza..
Hawa ambao wanaosema hawapigi kura wanaajenda yao na huwenda tayari wamepewa fedha ili wasije kur. Unawezaje kuja kukataa kupiga kura huku ukijua wazi kuwa usipopiga ni sawa na kubariki hiyo katiba, naamini watu watajitokeza kuja kupiga kura sasa wewe kama hutaki kwa nini usipige kura ya hapana,
Anasema watanzania wanadangaywa na huu umoja wa Ukawa na kusema khuenda wanalao wanalotaka kulitekeleza hivyo wakishiriki katika mchakato wa kura huenda mambo yasiwaendee vyema.
| Sehemu ya Jumuiya ya wanawake ya chama cha ADC wakifuatilia mada am bazo zilikuwa zinatolewa na mwenyekiti wa chama hicho Taifa Bw. Saidi Miraji Abdullah mapema hii leo |
No comments
Post a Comment