Zinazobamba

TMA YAPINGA KUPOTEZA BILIONI 1.2 KWENYE KODI,SOMA HAPA KUJUA

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini Dokta Agnes Kijazi
 akizungumza na Waandishi wa Habari leo
Jijini Dar es salaa

MAMLAKA ya Hali ya Hewa nchini(TMA) imekanusha taarifa zilizoandikwa na Vyombo mbalimbali vya Habari ambazo zilikuwa zinasema kwamba Mamlaka hiyo inapata Hasara ya bilioni 1.2 kwa mwaka kutokana na wao kupanga kwenye Jengo la Ubungo Plaza Jijini Dar es Salaam.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo
          Akikanusha Taarifa hizo Mkurugenzi wa Mamlaka ya Hali ya hewa nchini (TMA)Dokta Agnes Kijazi  leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema taarifa hizo sio za kweli zinalengo la kupotosha umma kwani ukweli uliopo ni kwamba Mamlaka hiyo imepanga kwenye ghorofa la tatu na la nne kwenye jengo la Ubungo Plaza na akabanisha   wanatozwa kodi ya milioni 132,kwa miezi mitatu  ambapo kwa mwaka mamlaka hiyo inalipa Milioni 528 sio Bilioni 1.2 .
           Aidha,Dokta Kijazi amesema kwa sasa Mamlaka hiyo iko mbioni kujenga jengo lao wenyewe ambapo tayali wameshapata kiwanja kilichopo Ubungo Jijini hapa na kwa sasa wako katika harakati ya kutafuta pesa kwa ajili ya kufanya ujenzi,na ameongeza kuwa pindi ujenzi ukikamilika itawasaidia katika kufanya kazi kwa uhuru kuriko sasa.
          Katika hatua Nyingine Mamlaka hiyo imetoa taarifa kuhusu Mvua za barafu zilizonyesha wiki iliyopita mkoani Kahama na kupelekea vifo vya watu 41 na kutokea  madhara ya kuharibika vitu mbalimbali ,ambapo amesema hali hiyo ya Mvua ni tukio geni hapa nchini na kusema inatokana na misiguano ambayo ipo katika wingu angani.

          Dokta kijazi akawataka wananchi wasipuuze taarifa zinazotolewa na Mamlaka hiyo,kwani taarifa wanazotoa zina ukweli na zitawasaidia wananchi kujikinga na majanga ambayo yanaweza kutokea kutokana na Mvua kali zinonyesha mara kwa mara.

 

Hakuna maoni