Zinazobamba

MFUMUKO WA BEI UMEONGEZA,SHILINGI YA TANZANIA YAZIDI ANGUKA,TAKWIMU YATAJA SABABU,SOMA HAPA KUJUA


OFISI ya Taifa ya Takwimu imesema Mfumuko wa  bei ykwa mwezi ulioisha wa pili umeongezeka  hadi asilimia 4.2 kutoka asilimia 4.0 ilivyokuwa mwezi January mwaka huu,Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo.
          Akitangaza Hali hiyo  Mkurugenzi wa Sensa za Jamii na Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Ephrahim Kwesigabo  leo Jijini Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema  Mfumuko huo wa Bei umeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo kwa mwaka ulioshia
         Aidha, Bwana Kwesigapo amesema kuongezeka mwa mfumuko wa bei wa mwezi Februari mwaka huu kumechangiwa na kuongezeka kwa bei za bidhaa zisizo za vyakula kwa kipindi kilichoishia mwezi Februari.
         Alibainisha kuwa Mwenendo wa bei za baadhi ya Bidhaa za Vyakula zilizoonyesha kuongezeka mwezi Februari  ni pamoja na bei za Mchele asilimia (18.5) unga wa muhogo (asilimia 9.3)nyama (asilimia 9.3),samaki asilimia 12.4 na maharagwe asilimia 7.1.
        Kwa upande Mwingine Bwana Kwesigapo Amesema Mwenendo wa Bei za bidhaa zisizo za Vyakula zilionyesha kuongezeka kwa mwezi Februari ikilinganishwa na mwezi huo huo kwa mwaka jana ni pamoja na mavazi ya Wanaume ambayo yameongezeka kwa Asilimia 4.7.mavazi ya wanawake asilimia 3.3,mkaa asilimia 5.1 mashuka  asilimia 3.1 pamoja na gharama za kumuona Daktari kwa asilimia 11.2.
            Kuhusu Thamani ya Shilingi ya Tanzania

Bwana kwesigapo amesema uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 64 na senti 59 mwezi februari ikilinganishwa na Shilingi 65 na senti 60 ilivyokuwa mwezi januari

Hakuna maoni