Zinazobamba

HABARI KUBWA LEO-KAFULILA AMBAMIZA KIKWETE,NI KUHUSU UFISADI WA ESCROW,AIPINGA KAFALA YA TIBAIJUKA SOMA HAPA KUJUA


MBUNGE wa Kigoma Kusini David Kafulila (pichani) ameendelea kuindama Serikali ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu Sakata ukwapuaji wa Mabilioni ya Shilingi  kwenye Akaunt ya Tegeta Escrow-
   Baada ya hivi sasa kuivaa tena serikali na kutaka iache ubabaishaji kwenye sakata hilo na  kuilazimishe iwataje kwa majina ya  Vigogo wa Ikulu walionufaika pesa kupitia Akaunt ya banki ya Stanbiki.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea Nayo hapo
       Kauli ya Mbunge kafulila inakuja ikiwa bado nchi wahisani wakiwa  wamegoma kutoa misaada kwa Serikali ya Tanzania wakitaka utekelezwaji wa Maazimio ya Bunge kwenye Sakata la ukwapuaji mabilioni ya Escrow.
        Nchi hizo wa hisani waliogoma ikiwemo Marekani kupitia Shirika la Millenium Challenge Corporation (MCC) ambao wamesitisha zaidi ya Sh.800 bilioni kwa awamu ya pili hadi mpaka kutekeleza maazimio ya Bunge kuhusu sakata hilo.
          Mbunge Kafulila alitoa kauli hiyo leo wakati alipokuwa anazungumza na Kituo cha Redio cha Magic Fm katika kipindi cha Morning Magic ambapo amesema kwa sasa kitendo cha Serikali kuwashtaki watu waliopewa pesa kupitia banki ya Mkombozi na kuwaacha waliochukua pesa kupitia akaunt ya Stanbiki ambao anadai wako vigogo wa Ikulu pamoja na Mawaziri ni kuwadanganya watanzania na kuficha ukweli.
            “tumepata taarifa kwamba waliochukua pesa kupitia banki ya Stanbiki wapo vigogo wa ikulu lakini leo serikali inaficha Suala hili na kuweka wazi majina ya watu waliochukua pesa kwenye banki ya mkombozi ,hata hivyo hii inaweka imani mbovu kwa serikali”amesema Kafulima.
        Kafulila  ambaye ni mtu aliyeliibua Sakata la Ufsadi wa Escrow Bungeni mwaka jana, ameongeza kuwa kama kungekuwa na serikali makini ingechukua hatua kali kwa viongozi  walioruhusu pesa kutoka pale Benk kuu (BOT) wakiachiwa.
     “Huyo Werema amehusika kwa kiasi kikubwa kuruhusu pesa kutoka ,muongo kama waziri leo  ameishia kujiuzulu wakati jina lake limehusika katika kutoka pesa lakini awachukuliwi hatua na tena hapa tunapata mashaka makubwa sana na hata kuhusika kwa ikulu kuchukua pesa kwenye Akaunt ya Stanbik hii inaoshesha wazi hakuna kinachotekelezwa”Ameongeza Kafulila.
Kuhusu nchi wahisani kugoma kutoa misaada kuhusu sakata hilo
           Mbunge Kafulila amesema nchi za wahisani wanajua sakata zima la escrow kuriko  watanzania wenyewe,huko akisema  Rais Kikwete haeleweki anavyowachukulia hatua watu waliopewa pesa kupitia benki ya Mkombozi.
          “Leo anavyowachukulia hatua watu waliopewa pesa na Rugimalira hata ujawakamata na hata Seth huyo singasinga hawachukuliwi hatua wala kupelekwa mahakamani,na mpaka leo huyo singasinga yupo tena bado anaendeleaa kumiliki mitambo hiyo huku TANESCO bado  wakilimpa billion tatu kwa mwezi,ndio maana nchi za marekani wanaona wazi hii,kwamba serikali haipo makini na tutakosa misaada tu’amesema Kafulila.
Alipouulizwa anazungumziaji kauli wanazotoa Viongozi waliopandishwa kwenye Baraza la Maadili ikiwemo kauli aliyoitoo Profesa Anne Tibaijuka kuwa Milioni kumi  ni hela ya mboga.ambapo kafulila amesema hizo ni kauli zinazoonyesha kwamba kuna ufisadi mkubwa hapa nchini.

“Kwamba watu wanaona ufisadi huu mkubwa wanashtuka,lakini wahusika wenyewe wa Ufsadi wanaona ufisadi wa kawaida ,kwani wanajua kunaufisadi mkubwa kuriko huu wa escrow ndio maana wanasema hivyo”

Hakuna maoni