Zinazobamba

TGNP YAZIDI KUWATETEA WANAWAKE,YAAZIMISHA SIKU YAO KWA KUTOA WITO MZITO,SOMA HAPO

Pichani Ni Mkurugenzi wa TGP Lilian Liundi akizungumza na Waandishi na Habari 

WITO umetolewa kwa Jamii kupinga vitendo vya Ukatili kwa wanawake nchini,ambavyo vimekuwa vikisababisha kuwepo kwa Watoto wa Mitaani.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo
        Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Kijinsia nchini TGNP Be Lilian Liundi wakati kuazimisha siku ya Wanawake Duniani ambayo iliazimishwa na TGP Ofisini Kwao ,ambapo Be Liundi amesema Lengo la maazisho hayo ni kutambua mchango wa  Mkubwa anofanya Mwanamke kiuchumi na Kimaendeleo hapa nchini.
     Aidha,amesema kuwa maadhimisho hayo yanatoa nafasi kwa mwanamke kutambua matukio mbalimbali yanayotokea ikiwemo kunyimwa haki zao za msingi kama vile kutogombea nafasi mbalimbali za uongozi Jambo ambalo limekuwa likisababisha wao kushindwa kupata nafasi hizo huku wakiwa na uwezo wa kufanya kazi hizo,
       Kwa Upande wake Mtetezi na Mwanahalakati Maarufu wa Wanawake nchini ambaye aliwai kuwa Mbunge na Waziri wa Elimu nchni Mama Thabitha Siwale amesema Bado Jamii imeshindwa kutambua mchango wa mwanamke huku ikizingia imepita miaka 20 baaa ya mkutano wa Bejing uliofanyika nchini China ambao umewapa nafasi wanawake lakini bado mfume dume unazidi kuwakandamiza.
Image result for full habari blog tngp
Washiriki mbalimbali waliojitokeza kwenye siku ya Wanawake Duniani

        Alibainisha kuwa Viongozi wanawake walioko katika Sekta za Maamuzi ya Sheria wanawajibu wa Kumtetea Mwanamke kwa kuziondoa sheria kandamizi kama yeye alivyokuwa Mbunge alivyofanikiwa kuondo kipengele cha Sheria kinachomyima Mwanamke kumiliki Ardhi.
      Vilevile Mama Siwale aliwataka wanawake kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali kwenye uongozi Katika chaguzi mbalimbali  Mwaka huu unaotarajiwa kufanyika Mwezi Octoba.

Maadhisho hayo ya Wanawake kwa Mwaka huu yana  kauli mbiu inayosema Uwezeshaji Wanawake,Tekeleza Wakati ni Siasa

Hakuna maoni