Zinazobamba

MKE WA KIKWETE MATATANI,AGEUZA ASASI YAKE KUWA MTAJI WA CCM,SOMA HAPA KUJUA



RAFU mbaya za Kisiasa zilizofanywa na Chama cha Mapinduzi CCM ndani ya Asasi inayohusu Masuala ya Maendeleo na kuwajengea uwezo( WAMA),Zazidi kuiweka Asasi hiyo Njia panda,Mtandao huu imedokezwa.anaripoti KAROLI VINSENT Endelea nayo
       Asasi hii ambayo  ilianzishwa mara tu baada ya Rais Jakaya Kikwete kuingia Madarakani mwaka 2005 na kupewa jina la wanawake na Maendeleo WAMA,na kutambulishwa kupitia jina la mke wa Rais Kikwete,Mama Salma Kikwete.
   Uchunguzi uliofanywa na Mtandao huu umebaini asasi hiyo imegeuka ya Wake wa Vigogo kutoka Ndani chama cha Mapinduzi,CCM na kugeuka kuwa miongoni mwa asasi inayofanya kazi ya  kuwaingiza madarakani Vigogo mbalimbali wa CCM,huku ikiwa kinyume na Matarajio ya wengi kwenye Asasi hiyo.
         Kwa mujibu wa sheria inayosimamia Asasi zisizo za Kiserikali nchini zinazuiliwa kwa Asasi kujiingiza katika masuala ya Kisiasa,lakini kwa asasi hii ya WAMA,inaonekana wazi kwenda kinyume kutokana kufanya kampeni ya Mgombea wa Urais mwaka 2010 kupitia CCM.
          Asasi hii imekuwa ikipigiwa kelele na Wabunge kutoka vyama upinzani nchini kwa kuishutumu kugeuka kuwa asasi ya chama cha Mapinduzi CCM.
   Kwa mujibu wa Vyanzo vya kuaminika ambavyo mwandishi wa Mtandao huu ameziona, zinaonyesha Jinsi Rafu ilivyofanyika katika Asasi hiyo kutokana Wajumbe wa Juu kwenye umoja huo wa Wanawake nchini,ambao ni Wake wa Viongozi na Makada kutoka CCM.
           Chanzo hicho kilionyesha kuwa, Mwenyekiti wa Asasi hiyo ni mke wa Rais Kikwete,mama Salma Kikwete,ambaye ni mjumbe wa Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM (NEC-CC)kutoka mkoa wa Lindi,
     Chanzo hicho pia kilimtaja Mjumbe wa Pili ambae ni Zakhia Meghji,huyu ambae ni mweka hazina Mkuu wa CCM na Mjumbe wa Kamati kuu cha hicho tawala ambacho ni chama pekee kikongwe ambacho kipo madalakani kusini mwa Jangwa la Sahala.
         Vilevile Meghji,amepewa ulaji mwengine na Serikali yake ya CCM na kwa kuchaguliwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumbe la Taifa NHC.
            Mjumbe mwengine wa Tatu,Mwanamwema Shein,mke wa Dk Ali Muhamedi Shein ambaye ni Rais wa Zanzibar na Makamo Mwenyekiti wa CCM
         Chanzo hicho kilizidi kutaja hujuma pamoja na Rafu inayofanywa na chama cha Mapinduzi kwenye Asasi hiyo kwa kumtaja Mjumbe wa Nne,ambaye Sophia Simba.Huyu ni Mwenyekiti wa Ummoja wa Wanawake wa CCM (UWT-CCM) .
      Sophia Simba,ambaye ni Waziri wa Maendeleo  ya Jamii,wanawake na Watoto.ambapo kisheria anapaswa kusimamia asasi zifuate maadili lakini ameshindwa kabisa kuisiamia Asasi ya Wama ambayo imekuwa ikijiingiza kisiasa.
    Mjumbe mwengine ni Regina Lowassa,mke  wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu mwaka 2007 kwa shinikizo la Bunge kufuatia kuhusika na ufisadi na Kashfa ya Mkataba wa Richmoond.
      Mume wa Regina vilevile ni Mbunge wa Munduli,ni mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Bunge la Tanzania,mbaye ni pia ni miongoni mwa watu wanaotumia kila aina ya njia kuhakikisha anakuwa Rais 2015.
      Rafu hii ilizidi kujidhilisha baada ya kubainika Mjumbe mwengine ambaye ni Blandina Nyoni kuwepo kwenye Bodi ya Wama.mama huyu aliwai kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya ambapo alisimamishwa kutokana kuzidisha ukilitimba ofisini.
      Duru zinasema Asasi hiyo,ambao iliazishwa kuwatetea wanawake kwa kuwaondoa kwenye lindi la Umasikini kwa kutoangalia upande wowote wa chama, lakini kwa sasa imeguka kuwa ni Asasi ya kuwaingiza wajumbe hao pamoja na wanaume zao kubaki Kula neema ya nchi kuliko kuwatetea wanawake.
       Kwa upande wake Mchambuzi wa Kisiasa na Msomi pia wa Masuala ya kisiasa kutoka chuo Kikuu cha Dodoma Seiph Yahaya alisema Hakuna Jipya kwenye asasi hiyo,na ipo kwa manufaa ya Tabaka Tawala tu.
“Sikiliza nikwambie,hapo hakuna kitu, tu hapo ni mpango wa kuhakisha wake waViongozi wanazidi kuneimeka tu,kwani kama Asasi hiyo ingekuwa inania Nzuri kwanini hakuna hata mjumbe yeyote kwenye bodi hiyo kutoka Chadema wala Cuf”
“Huu ni mwendelezo wa kutudanganya watanzania kwasabu washatujua sisi mazezeta sana,na hata mimi namshangaa sana waziri Sophia Simba na kushindwa hata kutetea sakata hili”alisema Seiph


Hakuna maoni