TGNP WAJA NA KAMPENI YA KUENZI MICHANGO YA WANAWAKE WALIOFANIKIWA
TGNP wametangaza kuwepo kwa KAMPENI ya kutambua na
kuenzi mchango wa wanawake katika historia ya Tanzania itakayozinduliwa 27
Machi mwaka huu jijini Dareslaam,
Akizungumza na Mtandao huu Ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania
(TGNP) Bi.Lilian Liundi amesema kuwa Lengo kuu la kampeni hiyo ni kuwaenzi wanawake
wote waliofanya vizuri katika kuleta maendeleo kuanzia ngazi ya jamii hadi
kitaifa bila kujali ukubwa wa mtu.
Liundi ameendelea kusema kuwa, Dhamira ya kuwaenzi
wanawake ambao wameonyesha mchango mkubwa kwa jamii inayowazunguka inatokana na
ukweli kuwa mpaka hakuna utamaduni wa kutambua michango ya mashujaa wetu
hususani wanawake
Katika kampeni hiyo itajikita katika kuwaenzi Wanawake
wote wakiwemo wale wanaojulikana na
wasiojulikana lakini wamekuwa hawatajwi mahali popote katika historia ya nchi
japo wana mchango mkubwa katika kuleta maendeleo na kutengeneza historia ya
nchi.
Kampeni itasaidia kutafiti na kukusanya taarifa
muhimu za michango ya wanawake katika maendeleo na historia ya nchi kijamii,
kiuchumi na kisiasa, na hivyo kuwafanya wanawake watambulike kitaifa na
kimataifa
Malengo mengine ni kuhamasisha wananchi kushiriki
katika kuibua na kutoa taarifa zilizopo na zitakazo kusanywa na kuzihifadhi
katika makumbusho na sehemu nyinginezo kwa njia ya digitali na makala;
Kutumia taarifa hizo kuwaenzi wanawake kama sehemu
ya kuhamasisha vizazi vya sasa na vijanvyo umuhimu wa ushiriki wa wanawake
katika maendeleo endelevu. Kuendeleza mijadala kuhusu michango na ushiriki wa
wanawake na kudai uelekezaji wa rasilimali kutoka kwa wadau mbalimbali katika
kuendeleza ushiriki wanawake na kuwaenzi.
“Kampeni itakuwa na awamu tatu. Kilele cha awamu ya
kwanza kitakuwa ni wakati wa tamasha la jinsia ambapo chapisho maalumu, makala
ya video, onyesho maalumu vitaandaliwa. zawadi mbalimbali kwa wanawake
watakaokidhi vigezo vinavyoonesha mchango mkubwa katika maendeleo na historia
ya nchi zitatolewa,” ameongeza Liundi.
Kampeni hiyo itachukua miaka mitatu. Inatarajiwa
kuhusisha wadau mbalimbali wakiwemo TGNP Mtandao, Makumbusho ya Taifa, Women
Research Development Project, Women Fund Tanzania (WFT), Soma na Shule ya
Uandishi wa Habari ya RAIDA pamoja na mashirika ambayo yanahusika katika
kutetea haki za wanawake na usawa wa kijinsia nayo pia yatahusishwa katika
kampeni hii.
No comments
Post a Comment