Zinazobamba

WAZIRI MKUU PINDA AUMBULIWA, JUKATA WASEMA KURA YA MAONI NI NDOTO KUFANYIKA

Kaimu mwenyekiti wa jukwaa la katiba Tanzania ndugu HEBRON MWAKAGENDA akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu  mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya ambapo amesema kwa uzoefu ambao wameupata huko Njombe unaonyesha wazi kuwa ni vigumu kwa kura ya maoni kuwepo, na kuwataka serikali wasione haya kusema kuwa zoezi hilo ni ndoto kuwezekana
Sehemu ya wanahabari wakisikiliza kwa makini, hoja za makamu mwenyekiti wa jukwaa la katiba,
Mwanashiria Kutoka kituo cha sheria na haki za binadamu Bi GERINE FUKO akizngumzia kisheria juu ya mchakato wa kura ya maoni  ambapo amesema kuwa katika kuelekea mchakato huo wa upigaji wa kura ya maoni ili kupata katiba mpya imebainika kuwa sheria ya kura ya maoni ina mapungufu makubwa ambayo yanaweza kusababisha upigaji kura ya maoni ukaingia dosari kubwa
Mdau akiwa kazini mapema hii leo.
 Kukiwa na kauli za sintofahamu ambazo zinatolewa naviongozi wa ngazi za juu akiwemo waziri mkuu wa Tanzania, Mh. Mizengo Kayanza Petter Pinda kuhusu kura ya maoni, jukwaa la katiba limeibuka na mambo makubwa yaliyowashangaza wanahabari,
JUKWAA hilo la katiba wameibuka upya baada ya kukaa kimya kwa muda na sasa wamekuja na tamko kali kwa selikali, wakiitaka kuacha mara moja nia yao ya kutaka kutumia daftari la zamani kutumika katika upigaji wa kura ya maoni inayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi wanne

Tamko hilo limekuja kufuatia habari za kuaminika ambazo Jukwaa la katiba imezinasa zikisema serikali inajiandaa kuendesha kura ya maoni kama ilivyotangazwa na rais kwa kutumia daftari la kudumu la wapiga kura la zamani, suala ambalo wanasema halikubaliki,

Akizungumza na mwandishi wa mtandao huu mapema hii leo, Kaimu mkurugenzi wa  jukwaa hilo, Bw. Hebroni Mwakagenda, amesema tayari wamepata taarifa hizo na kudai kuwa hatua hiyo inafikiwa ikiwa ni nia ya serikali kutaka kulazimisha kura hiyo ya maoni kufanyika katika tarehe iliyotangazwa,

Mwaka genda ameendelea kusema kuwa, kwa mujibu wa taarifa za ndani toka tume ya taifa ya uchaguzi (NEC)iliyotolewa na mwenyekiti wake, Jaji mstaafu Damian Lubuva zinasema daftari hilo la kudumu la mpiga kura kwa sasa halitamaniki, kwani limechafuka vibaya mno kiasi cha kutoweza kurekebishika na kutumika tena kwa kura ya maoni ya April 30,2015 kama ilivyotangazwa na rais.

Aidha, mwenyekiti huyo amebainisha uwezekano hafifu ambao uliopo wa kufanyika kwa kura ya maoni, kwa kusema mpaka hivi sasa mchakato wa kura hiyo uko katika mkwamo, kuanzia zoezi zima la uandikishaji, kutoa elimu, na hata kupiga kampeni kwani mpaka hivi sasa siku zimebaki takribani 36 ambazo hazitoshi kwa mchakato kukamilika,

Ameiomba serikali kuangalia upya sakata hilo, katika mwelekeo wa kuahilisha , ili kutoa fursa kwa michakato mingine kufanmyika ikiwemo uchaguzi mkuu wa oktoba ambao hivi sasa joto lake tayari limeshapanda

Akitaja sababu za kuahirisha  mchakato huo kwa wanahabari wanahabari mapema leo jijini Dar es salaam kaimu huyo  mwenyekiti wa jukwaa  amesemani kusuasa sua kwa zoezi la uandikishwaji wa daftari la kudumu kwa mfumo mpya wa BVR,

Amesema hiyo ni  ishara tosha kuwa ni ndoto kwa Tanzania kupata katiba bora kwani hadi sasa kuna idadi kubwa ya wananchi ambao hawajajiandikisha katika daftari hilo huku muda wa kupiga kura hiyo ukiwa unakaribia jambo ambalo limekuwa likimtatiza kila mtanzania kama jambo hilo linawezekana.

Amesema kuwa kutokana na upungufu wa vifaa pamoja na rasilimali nyingine unaoonekana wazi katika zoezi hilo ni wazi kuwa daftari hilo haliwezi kukamilika na kutumika katika kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa

Akizungumzia zoezi  ambalo lilifanyika katika miji ya makambako na njombe la uandikishwaji wa daftari  la mpiga kura limeonekana kuchukua zaidi ya miezi miwili kukamilika ambapo amehoji ni vipi  zoezi hilo linaweza kufanyika kwa tanzania nzima ndani ya kipindi kifupi na kufanikisha  kwa zoezi la upigaji kura ambao umepangwa kufanyika tarehe 30 mwezi wanne mwaka huu.

Pinda alikaririwa na vyombo vya habari mbalimbali akisema kura ya maoni iko palepale, na watu wawe tayari kwenda kujiandikisha ili wapate fursa ya kuandika katiba inayopendekezwa.

No comments