HABARI KUBWA-MKE WA DK SLAA AMUENYESHA KAMANDA KOVA,AHOJIWA KWA SAA TATU.SOMA HAPA

MKE wa
Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dokta Wilbroad Slaa,
mama Josephine Mshumbuzi amejisalimisha kwenye Jeshi la polisi Kanda maalum ya
Dar es Salaam na kushikiliwa kwa zaidi ya saa tatu kwa mahojiano.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Mama Mshumbuzi amejisalimisha leo makao
makuu ya Jeshi la polisi kanda hiyo ili kutoa ushahidi juu ya tuhuma
zilizoibuliwa na Chadema kuhusu mipango ya kumuua katibu huyo wa chadema ambazo
wanadai kusukwa kwa ustadi mkubwa na Aliyekuwa Mlinzi wa Dokta Slaa, bwana
Khalid Kagenzi pamoja-
Na kaimu mkuu wa Usalama wa Taifa wa wilaya
ya kinondoni Elisifa Ngowi
pamoja na vigogo mbali mbali wa Chama cha Mapinduzi CCM.
Mwanamama Mshumbuzi aliwasili polisi
majira ya saa nne asubuhi leo huku akiongozana na viongozi mbalimbali wa
Chadema,katika mahojiano hayo yaliyodumu zaidi ya saa tatu yanatajwa yalikuwa
yanalengo kuchua ushahidi juu ya tuhuma hizo za mauaji.
Kujisalimisha
huko kwa Mke wa Dokta Slaa kunakuja ikiwa teyari jeshi hilo la polisi kanda ya Dar es Salaam limeutangazia
ulimwengu kwamba idara ya Usalama wa
Taifa kutohusika kwenye madai ya mipango ya kumuua Dokta Slaa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Kanda Maalum ya
Dar es Salaam Kamishna Suleiman Kova waliwambia wanahabari wiki iliyopita kwamba katika sakata
hilo watahojiwa watu wote ambao wametajwa kuhusika kutaka kumuua Dokta Slaa ila
kasoro usalama wa Taifa.
No comments
Post a Comment