DC MAKONDA AMVAA ASKOFU GWAJIMA,ATANGAZA KIAMA NAYE SOMA HAPA KUJUA

NA KAROLI VINSENT
SIKU moja
kupita baada ya jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es Salaam kutangaza
kuwakamata watu 15 ambao waliokuwa wakitaka kumtorosha Askofu wa Kanisa la
Ufufo wa Uzima Josephat Gwajima ambaye
amelazwa katika Hospitali ya TMJ, Mikocheni Dar es Salaam kutokana kuugua gafla
akiwa kwenye mahojiano na Jeshi la polisi
Naye Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni Paul Makonda (pichani) ameibuka na Kumtaka Askofu Gwajima kujisalimisha ofisi kwake mara moja kabla hajamchukuli hatua
kali za kisheria
Kauli hiyo ya Makonda ameitoa leo
jijini Dar es Salaam wakati wa akizungumza na mtandao huu ambapo amesema tayari
ameshatoa maagizo kwa askari wake zaidi ya ishirini kumtafuta Askofu huyo
popote alipo ilia achukuliwe hatua kali kutokana na madai anayodai kwamba kiongozi
huyo wa kiroho anamiliki silaha kinyume na taratibu.
“Mimi teyari nimewaagiza askari wangu
wamtafute popote alipo na wamfikishe ofisini kwangu ili mkondo wa sheria
uchukue hatua kali,Maana sababu ya kumtaka ajisalimishe kwangu inatokana na
kubaini –“
“Askofu huyu anamiliki Bastora kinyume na taratibu tena
hata mimi mkuu wa wilaya ambaye ndio mwenyekiti wa ulinzi wa wilaya hii sina
taarifa,”amesema Makonda.
Makonda ameongeza kuwa mbali na kumiliki
Bastora hiyo pia amedai kwamba kiongozi huyo wa dini ametoa maneno ya
kumkashifu Askofu wa Kanisa katoliki jimbo kuu la Dar es Salaam Mwadhama
Kardinali Polycarp Pengo ambapo amesema kauli hiyo inalengo la kuharibu
na kuvunja amani ya nchi.
Aidha,Makonda ameendelea kusema kwamba
endapo askofu hiyo akikaidi kujisalimisha ofisini kwake basi ajiadhari
kutafutwa kwa kunguvu na kuchukuliwa hatua kali.
“Mimi ni mtu makini sana na hata chama changu
wananijua na misimamo yangu kabisa na huwa sipendi kuyumbishwa namuomba Askofu
Gwajima asilete utoto wa kupuuza maagizo yangu maana nitamchukulia hatua kali
za kisheria”ameongeza Makonda
Kauli ya Makonda inakuja ikiwa siku moja
kupita baada maaskofu na waumini wa kanisa hilo kutoka mikoa mbalimbali, kuwasili
jijini Dar es Salaam ili kufuatilia afya ya kiongozi wao.
Waumini hao walianza kujitokeza jana saa 2 asubuhi katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe ambako ndiyo makao makuu ya kanisa hilo.
Hali katika uwanja huo, ilikuwa tulivu huku ulinzi ukiwa umeimarishwa na watu wote ambao walionekana si waumini wa kanisa hilo, wakiwamo waandishi wa habari wakibainika mapema.
Ilipofika saa 5:30 asubuhi, Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Gwandu Mwangasa alianza kuwatambulisha maaskofu na wawakilishi waliotoka mikoa mbalimbali ili waweze kutambuliwa na waumini wenzao.
Mchungaji Mwangasa, aliitaja mikoa ambayo viongozi na maaskofu wamefika Dar es Salaam kuwa ni Lindi, Geita, Shinyanga, Mwanza, Morogoro na Iringa.
Mikoa mingine, ni Singida, Arusha, Tabora, Njombe, Tanga na Dodoma.
Katika ibada hiyo, baadhi ya waandishi wa habari na wapiga picha walifukuzwa na viongozi wa kanisa hilo kwa madai kuwa hawana kibali cha kuwepo mahali hapo.
Waumini hao walianza kujitokeza jana saa 2 asubuhi katika viwanja vya Tanganyika Packers Kawe ambako ndiyo makao makuu ya kanisa hilo.
Hali katika uwanja huo, ilikuwa tulivu huku ulinzi ukiwa umeimarishwa na watu wote ambao walionekana si waumini wa kanisa hilo, wakiwamo waandishi wa habari wakibainika mapema.
Ilipofika saa 5:30 asubuhi, Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo, Gwandu Mwangasa alianza kuwatambulisha maaskofu na wawakilishi waliotoka mikoa mbalimbali ili waweze kutambuliwa na waumini wenzao.
Mchungaji Mwangasa, aliitaja mikoa ambayo viongozi na maaskofu wamefika Dar es Salaam kuwa ni Lindi, Geita, Shinyanga, Mwanza, Morogoro na Iringa.
Mikoa mingine, ni Singida, Arusha, Tabora, Njombe, Tanga na Dodoma.
Katika ibada hiyo, baadhi ya waandishi wa habari na wapiga picha walifukuzwa na viongozi wa kanisa hilo kwa madai kuwa hawana kibali cha kuwepo mahali hapo.
No comments
Post a Comment