Zinazobamba

MAKONDA AANZA NA 'BONGO STAR SEARCH' YAKE KINONDONI SOMA HAPA KUJUA


MKUU wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda (pichani)amezindua shindano la “Kinondoni Talent Search”ambao ni mpango wa wenye lengo la kutambua vijana wenye vipaji mbalimbali ili kuwapatia nafasi.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
           Makonda amezindua Shindano hilo leo Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na vyombo mbalimbali vya habari ambapo amesema shindano la Kinondoni Talent Search lina lengo la kuwatengenezea nafasi ya mafanikio vijana wenye vipaji ,kuwapatia mafunzo muhimu ikiwemo kuwaunganisha na wadau mbali mbali.
         Makonda ameongeza kuwa Shindao hilo ambalo litachukua  mwezi mmoja na nusu ambapo litashirikisha kata zaidi ya 30 zilizopo wilaya ya Kinondoni.
         Aidha ,Makonda amesema katika hatua za kuwatafuta vijana hao wenye vipaji, shindano hilo litasimamiwa na Jumanne Mrimmy ambaye ni Afisa utamaduni wilaya ya kinondoni,Sebastian Mhowera afisa Habari wa manispaa hiyo.
         Mbali na viongozi wa Wilaya hiyo pia manispaa hiyo imewahusisha wasanii mbali mbali ambao ni Peter Msechu,Jokate Mwegelo pamoja na Mc anayetamba hapa mjini ambaye anatamba na mambo ya uchekeshaji maarufu kwa jina Mc-Pilipili.

          Vilevile Makonda amewataka Vijana kujitokeza kwenye mashindano hayo yanayoanza hivi sasa na kujitokeza kwenye kata zao zilipo wilaya,amesema mashindano hayo yanalengo la kuwatoka katika hali ngumu ya maisha.

No comments