HABARI KUBWA LEO-LOWASSA AWAPONZA WANAFUNZI UDOM,UONGOZI WAANDAA PANGA,WANAFUNZI WENGINE WAWASUTA,SOMA HAPA
UONGOZI wa
chuo Kikuu cha Dodoma unaangalia uwezekano wa kuwachukulia hatua kali za
kinidhamu wanafunzi wa chuo hicho walioandamana mpaka nyumbani kwa kada wa
chama cha Mapinduzi CCM Edward lowassa kwa kumtaka agombee Urais hapo baadae mwaka huu.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea.
Wanafunzi hao wa shahada za juu kutoka
chuo hicho waliandamana mwanzoni mwa wiki hii kwenda nyumbani kwa lowassa
wakiwa na mabango pamoja pesa ambazo
wanadai wamechangishana na kumpatia Lowassa ili itumike kwenye gharama za
kuchukulia fomu ya kutaka nafasi ya Urais ndani ya chama cha mapinduzi CCM.
Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu aliyoko
kwenye chuo kikuu hicho anasema kwa sasa viongozi wa juu wa chuo hicho
wanatafakali na kuangalia ni hatua gani watachukua kwa wanafunzi waliokwenda
kwa Lowassa.
“Kusema kweli wanafunzi hawa
wametufedhesha sana kwa utoto huu waliofanya,yaani wamekihaibisha chuo hichi
ambacho kinasifika kwa kutoa elimu hapa nchini,na tangu jana walivyoenda huko
Makamu mkuu wa chuo hichi amekasirika sana na uwenda akachukua hatua za
kinidhamu kwa wanafunzi hawa”kimesema Chanzo chetu.
Lowassa ambaye aliwai kuwa waziri mkuu
ambapo alijiuzulu kutokana na yeye kuhusika kwenye ufisadi mkubwa ambao unalighalimu
taifa mpaka leo kwenye Kampuni tata ya kufua umeme ya Richmound ambaye sasa
anatajwa ni miongoni mwa makada wa Chama cha Mapinduzi CCM ambao wanaoutaka
Urais kwa udi na Uvumba.
Mtoa taarifa mwengine kutoka chuo hicho
ambaye yeye anatoka kwenye ofisi ya taaluma ameuambia mtandao huu kwamba kama
chuo makini hakiwezi kufumbia kile anachokiita ni utovu wa ni Nidhamu wa hali
ya juu kwa wanafunzi kuacha kusoma na kujiingiza kwenye masuala ya siasa.
“sisi wenyewe leo tulitegemea labda
ofisi ya mawasiliano ya (UDOM) ingetoa Tamko kuhusu hatua ya wanafunzi hawa kwa
njaa zao kuwafuata watu mafisadi,harafu
sijui kwanini viongozi,wanaangalia ila nimesikia chuo wanaangalia hatua zipi
watachukua maana kama tukiacha kitaonekana chuo ambacho kinazalisha wanasiasa
wenye kutafuta pesa na sio wasomi bara wa hizo siasa na masomo mengine”amesema.
Kuibuka huko kwa baadhi ya wanafunzi
wa Chuo hicho kutoa matamko au kufanya mambo yanayooneka ni ya kama ya kisisa
yamekuwa yakijirudia mara kwa mara ikumbukwe kwenye sakata la Ufisadi wa Escrow
wanafunzi wa chuo hicho walitoa tamko la kumtaka Rais Kikwete awachukulia hatua
viongozi walioingiza nchi kwenye ufisadi huo.
WANAFUNZI WENZAO WA UDOM WANENA.
Nao baadhi
ya wanafunzi wa chuo hicho waliozungumza na mtandao huu kwa sharti la kutotaja
majina yao wala kozi wanazosoma,wameonesha kuchukizwa na kitendo cha wanafunzi
wa chuo hicho kwenda kwa Lowassa.
“Mimi nashangaa sana nchi nzima
kunavyuo vikuu vingi sana mbona hatuwaoni kujiingiza kwenye utoto huu,yote haya
yanatokana na uongozi wa chuo chetu kuendelea kuuuwafumbia macho wanafunzi hawa
ambao wanawaza pesa tu”
Kwa upande wake mwanafunzi mwengine
amesema kwa kufichua mchezo mchafu ambao anadai hata pesa waliomkabidhi Lowassa
imetoka kwa makundi la Lowassa.
“Yaani huyu
jamaa sijui anang’ang’ania nini huku Ikulu yaani anayekwambia hata hizo pesa ni
za kwao hao wanafunzi ni muongo bwana hizo pesa zimetoka kwa mtu bwana Ipson
ambaye ni mtu wa lowassa na amempa (anamtaja jina”ndio kiongozi wa chuo hichi
ambao wanaapa kumuunga mkono Lowassa”
WANAFUNZI WA VYUO VINGINE WANENA.
Kwa upande wao wanafunzi wa vyuo vingine
nao hawakuwa nyuma kuzungumzia hatua hiyo ya wanafunzi wenzao wa chuo kikuu cha
Dodoma.
wakwanza alikuwa ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania Israel Mwalenge naye amesoneshwa na kitendo cha wanafunzi hao kwa kusema wanakifedhehesha chuo.
wakwanza alikuwa ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu Huria Cha Tanzania Israel Mwalenge naye amesoneshwa na kitendo cha wanafunzi hao kwa kusema wanakifedhehesha chuo.
“Hata mimi
nashangaa sana,lakini inaonekana uongozi wa chuo hicho hawako makini,hivi
wanavyofanya hivyo wanakishusha chuo hicho kikubwa hapa nchini”amesema Mwalenge.
WANAFUNZI WENYEWE HAO HAPO WAKIENDA KWA LOWASSA
WANAFUNZI WENYEWE HAO HAPO WAKIENDA KWA LOWASSA
Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiwasalimia mamia ya wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu mkoa wa Dodoma, waendesha boda boda na wamachinga wa mkoa huo walioandamana hii leo hadi nyumbani kwake Area D mjini Dodoma kumuomba pindi wakati ukifika kwa mujibu wa taratibu za chama cha Mapinduzi (CCM) asisite kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais.
Lowassa amesema anazidi kuhamasika kufuatia maombi ya watu wa makundi mbalimbali ya jamii wanao muomba kugombea urais mwaka huu.
Aidha na yeye amewaomba vijana hao na makundi mengine kuwahimiza wenzao vyuoni na hata mitaani kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura ili siku ya uchaguzi wawe na sifa za kuweza kushiriki katika uchaguzi kwa kupiga kura.
Rais wa serikali ya wanafunzi akizungumza
Mheshimiwa Lowassa akizungumza na wanachuo hao
Wanafunzi hao zaidi ya 300 walifika nyumbani kwake hapo majira ya saa sita mchana na kuzungumza nae na kufikisha salamu zao ikiwa ni pamoja na kumchangia fedha za kuchukulia fomu.
Aidha Lowassa kwa Upande wake amewashukuru vijana hao na kusema kuwa ujio wao na ule wa masheikhe wa Bagamoyo unazidi kumhamasisha kutangaza nia na pindi muda ukifika anaweza kufanya hivyo.
Walibeba na mabango yaliyo na jumbe mbalimbali
Bodaboda nao walifika eneo hilo
Sehemu tu ya umati uliofika nyumbani hapo kwa Lowassa hii leo.








No comments
Post a Comment