Zinazobamba

EXLUSIVE-GAZETI LA MBOWE LAMALIZWA TENA,CHAMA CHA ACT YAIBOMOA GAZETI LAKE SOMA HAPA KUJUA

Freeman Mbowe


KAMA ni Majanga basi ndio yanayolikuta gazeti  la Tanzania Daima ambalo  linamilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema,Freeman Mbowe,baada ya hivi sasa kukimbia na lundo la wahariri na waandishi wake wa Habari, ambapo sasa mwandishi wake muhimu Abdallah Khamis amehama rasmi gazeti hilo linalotoka  kila siku.Anaandika KAROLI VINSENT  endelea nayo.
          Taarifa za kuamika ambazo mtandao huu umezipata zinasema kwa sasa ni wazi gazeti hilo limekuwa likipungukiwa waandishi  wake  baada ya Mwandishi muhimu Abdalla Khamis kulitema gazeti hilo na kwenda kwenye chama kipya cha siasa cha ACT-Tanzania na kuukwaa nafasi ya Afisa Habari wa chama hicho.
           Kwa mujibu wa Mtoa taarifa wetu aliyoko ndani ya Gazeti la Tanzania Daima anasema kwa sasa gazeti limekuwa likipitia katika kipindi kigumu,ambapo anadai kuondoka  kwa Abdallah Khamis ni wazi sasa gazeti hilo linaingia kwenye kipindi kigumu.
Pichani  ni Abdallah Khamis
         “Yule bwana Khamis ni mwandishi mmoja ni mzuli sana tena mimi  kama mwandishi mwenzake nasikitika sana kwa uongozi kumwacha mwandishi huyo aondoke kirahisi hivyo,maana ukizungumzia Abdalla unazungumia kiungo muhimu sana na sijui hatma ya gazeti baada ya kuhama yeye”ametupasha mtoa huyo taarifa.
           Mtandao huu umenasa barua ambayo imethibitisha ni wazi amekuwa Afisa Habari wa ACT-Tanzania,kwa mujibu wa Barua hiyo  ambayo yeye Abdallah alikwa akiwataarifu waandishi mbalimbali wa vyombo vya Habari kwamba chama cha ACT-Tanzania[FPM1]  kitakuwa na Mkutano mkuu ambao unaotarajia kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
Ambapo barua hiyo inasomeka hivi  
“Chama cha ACT-Tanzania kitafanya Mkutano wa Halmashauri Kuu,Kamati kuu na Uzinduzi wa Chama kuanzia machi 27-29/2015 Kutokana na umuhimu wa chombo chako katika kuupatia umma wa Tanzania habari sahihi, tunakaribisha uwakilishi kutoka kwako katika shughuli hiyo. Tunaomba mtupatie majina ya waandishi na wapiga picha watakaohudhuria matukio hayo kwa siku hizo tatu. Asante kwa ushirikiano wako Abdallah Khamis Afisa Habari”.
        Nafasi hiyo ya Afisa habari wa chama hicho ilikuwa ikishikiliwa hapo awali na Karama Kaira,ambaye haijasemekana mara moja amepewa nafasi gani ndani ya chama hicho kichanga cha siasa nchini.
     Kuhama huko kwa Mwandishi huyo kunazidi kuliacha gazeti la Tanzania Daima katika wakati mgumu ambapo wiki chache zilizopita Gazeti hilo liliondokewa na Mhariri wake muhimu Edson Kamukara ambaye ametimkia gazeti la Mawio,
           Mbali na Kamukara wahariri wengine waliolikacha Gazeti hilo ni Amana Nyembo ambaye nae ametimkia Gazeti la Mwananchi na kuwa sub editor.
       Mhariri mwengine aliondoka Gazeti hilo aliyekuwa Mhariri Mtendaji  Ansbert Ngurumo ambayo naye ametangaza kuachana na gazeti hilo ambapo inasemekana anajiaadaa kugombania Ubunge hapo kwenye uchaguzi mkuu hapo baadae kwenye mikoa ya kanda ya ziwa na Nafasi yake kujazwa na kwenye Gazeti hilo ikajazwa na  Neville Meena,ambaye alikuwa Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi
   Waandishi waliohama.
Achia mbali Wahariri,kuna waandishi mbalimbali waliohama hivi karibu ni Shaban Matutu ambaye amehamia Gazeti la Mtanzania na Lucy ngowi aliyehama hivi karibuni.
Wengine waliohama ni Bwana Maziku aliyehamia kwenye Kampuni inayohusika na kusimamia magari ya Uda na kuwa afisa habari.






Maoni 3

Elias Ibrahim Mhegera alisema ...

kuhama kwa waandishi na wahariri i jambo la kawaida sana

Unknown alisema ...

Sasa hapo pigo liko wapi acheni propaganda zenuu hapaa

Andrew Chale alisema ...

Mweee? mbona habari haina kichwa wala miguu? ama ulikuwa unataka kutangaza huo mkutano a ACT kiujanja kwa kupitia njia ya kuama mwandishi?. Jamani wewe unamiliki blog, hivto chunga sana kuandika habari ambazo hazibebi kichwa na masikio bali zile zinazobeba akili na maarifa. SAWA SAWA.!! SUALA LA KUHAMA NI LA KAWAIDA HAKUNA MTU ANAYEKAA MILELE HASA KENYWE HII TASNIA YA HABARI. Mbona mimi nimehama Tanzania Daima? na nilikuwa nalo tokea 2007 hadi 2015, mwanzoni? nimeama na kwenda kwenye blog. Mtu anahama kwa mapendekezo yake na wala kuondolka si pigo kwani wapo na walikuapo zaidi yake..