Zinazobamba

BODABODA WAZIDI LILIWA,NI KUHUSU BIMA YA AFYA,MBUNGE MWAIPOSA ASEMA YAKE SOMA HAPA KUJUA


WITO umetolewa kwa Waandesha pikipiki Maarufu  “Bodaboda”Kujiunga na Huduma za Bima ya Afya ili iwasaidie pindi wanapopata Ajali ambazo zimekuwa zikiongozeka kila Kukicha.Anaandika KAROLI VINSENT Endelea nayo hapo

      Wito huo umetolewa mda huu Jijini Dar es Salaam na Afisa mtekelezaji wa Mfuko wa Bima ya Afya Bwana Goefrey Tumain wakati ya Semina ya siku moja kwa Madereva  bodaboda walioko Jimbo la Ukonga Jijini hapa ambapo Bwana Tumain amesema Bodaboda wengi wamekuwa wakitesaka sana pindi wapatapo ajali huku wakisota kwa kukosa matibabu kwasababu hawako kwenye huduma ya Bima ya Afya.
        Bwana Tumain ameongeza kuwa kwa sasa Mifuko ya Bima ya Afya imewapa nafasi bodaboda ambao watajiunga kwenye vikundi vyao kwa kutoa pungufu ya kulipia Gharama ya Elfu 76800 kwa mwaka.
        Amebainisha kuwa  Bodaboda ambao hawapo kwenye Vikundi watatozwa Gharama ya tofauti ambayo ni Laki tisa kwa mwaka.
           Kwa Upande wake Mbunge wa Jimbo la Ukonga Eugin Mwaipopo amewaomba Bodaboda kutii sheria zilizowekwa na Mamlaka husika  na ameitaka Serikali kuangalia upya zuio waliloweka kwa Bodboda kutoingia katikati jiji kwa kusema kwamba kunawarudisha nyuma kwenye maendeleo bodaboda hao kwakukosa pesa.

        Vilevile Mbunge huyo amesema kitendo cha kuwazuia kwenda mjini kutasababisha kuongezeke kwa vitendo vya wizi kwenye maeneo mbalimbali huko ikifamika kwamba madereva hao wa Bodaboda wamekopa pesa kupitia sehemu mbalimbali.

Hakuna maoni