Zinazobamba

RAIS KIKWETE KUBULUZWA UN,MALBINO WACHACHAMAA,WASEMA WAMEMCHOKA SOMA HAPA KUJUA

Pichani ni Msemaji wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Torner

CHAMA cha Albino Tanzania (TAS), kimetoa miezi mitatu kwa Rais Jakaya Kikwete kuingilia kati vitendo vya mauaji ya albino yanayoendelea nchini. Akishindwa kuchukua hatua, watamshitaki Umoja wa Mataifa (UN). Anaripoti Sarafina Lidwino … (endelea).
Akizungumza na CHANZO Changu, Afisa Habari wa TAS, Josephat Torner amesema, wamechoshwa na vitendo vya mauaji ya albino vinavyoendelea huku Rais Kikwete akiwa kimya.
Torner amesema Rais Kikwete ni rais wa Watanzania wote hivyo analazimika kukomesha mauaji ya albino na akishindwa kuchukua hatua katika kipindi hicho walichompa watapeleka malalamiko yao UN.
Alisema watalazimika kufika huko kwani chama chao kimesajiliwa chini ya UN hivyo wakishindwa kusaidia wa Rais Kikwete watalazimika kukimbilia huko ambako wana imani watasaidiwa.
Msemaji huyo alisema kabla ya kupeleka malalamiko yao UN watafanya maandamano makubwa Machi 2, 2015 nchini nzima, na kwa upande wa Dar es Salaam wataanzia Ocean Road na kumalizikia Ikulu ambapo wamepanga kumuona Rais Kikwete na kumpa malalamiko yao.
“Maandamano hayo ya amani yatakuwa na kauli mbiu ‘MAUAJI YA ALBINO SASA BASI’. Mikoani Albino wataandamana kwenda ofisi za wakuu wa mikoa kupeleka vilio vyao,” alisema Torner.
Tangu mwaka 2006 zaidi ya Albino 76 wameuawa, na majeruhi waliopo ni zaidi ya 56 na makaburi 18 yamefukuliwa na kuchukuliwa miili ya waliozikwa huku walioachwa na ulemavu wa kudumu ni 11, hakuna muuaji hata mmoja aliyekamatwa.
Chanzo ni Gazeti la Mwanahalisi.online

Hakuna maoni