Zinazobamba

HABARI ILIYOTIKISA JIJI-KIMENUKA CCM,MAKADA WAKE WAAPA KUFA NAE MAKONDA,WASEMA MAZITO SOMA HAPA KUJUA

    
Pichani n Mwenyekiti wa zamani wa chama hicho Mkoa wa Singida na Kada maarufu wa chama hicho Bwana John Guninita
Akizungumza na Waandishi wa Habari Mda huu jijini Dar es Salaam
Picha na Exaud Mtei

KILE kinachoonekana kwamba hali ya kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM imekuwa sio shwali baada ya Mwenyekiti wa zamani wa chama hicho Mkoa wa Singida na Kada maarufu wa chama hicho Bwana John Guninita ameibuka na kusema atambuluza mahakamani –
Katibu wa vijana na  uhamasishaji wa Chama cha Mapinduzi CCM Paul Makonda mahakamani.Anaripoti KAROLI VINSENT Endelea nayo.
        Makonda ambaye sasa ni Mkuu wa Wilaya wa Manispaa

ya Kinondoni anatuhumiwa na Guniinta kutokana na kitendo chake cha kumtukana na kumuita yeye mtu anayetumiwa na kada anayetaka Urais kwa udi na uvumba kutoka ndani ya chama hicho Edward lowassa.
        Hayo yametangazwa na Guninita mda huu jiji Dar es Salaam wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari Ambapo Mwenyekiti huyo wa zamani huku akiongozana na Mwanasheria wake ambapo amesema hawezi kuvumilia unyanyasaji na uonevu anaofanyiwa huku viongozi wa juu wa Chama hicho wakimfumbia macho.
            “leo kijana mdogo kama makonda mtu ambaye ukimwangalia ni mdogo sana kisiasa hata mimi anaifikii kwa ukongwe wangu wa siasa leo ananitukana na mamlaka zinamwangalia sasa mimi najiuliza hiki chama chetu kinauongozi kweli?,mimi siwezi kukubali kama wao viongozi wajuu wanamwachia kwa maslai nao mimi ila siliogopi nasema naenda mahakamani na nahakikisha nitamfunga”amesema Guninita.
         Guninita ameongeza kuwa madai anayodai yeye, hayuko peke yake bali yuko na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida bwana Sindai na amesema kwa sasa haoni haja ya kumsubili na kuwachia aendelee kumtukana mitaani.
Kuhusu Kumpiga Jaji warioba.
Gunita amesema anashangaa sana kijana huyo kumevunjia heshima kutokana na kitendo chake cha kumpiga jaji warioba na kupewa ukuu wa wilaya.
     “Kama chama makini leo kisingempa hata nafasi ya ukuu wa wilaya maana mtu amempiga Jaji warioba leo anapewa vipi Ukuu wa wilaya huku akimfanyia vitendo vya kiovu kama kile,harafu anajitetea na kwa kusema alikuwa mlinzi wa wake hivi mtu  hana sifa ya kuwa mlinzi warioba wakatio ukweli ni huu yeye amempiga warioba na hatufai kabisa kama mnataka muone nampeleka mahakamani”alisema Guninita.
  

          Alipoulizwa na Waandishi wa Habari kwanini madai yake asipeleke kwenye Kamati za maadili za chama hicho Guninita alijipu hawezi kufanya hivyo kutoka na kitendo chake kinaonyesha wazi ni kosa la jinai.

Hakuna maoni