Zinazobamba

FREEMAN MBOWE ALIPUKA,NI KUHUSU UCHAGUZI 2015,ASEMA NENO KALI SOMA HAPA KUJUA





Freeman Mbowe
Pichani ni Freeman Mbowe picha na Maktaba
Chama  Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimejipanga kuhakikisha katika uchaguzi Mkuu hawaibiwi kura.

          Kauli hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa chama hicho, Freemon Mbowe  wakati akizindua mafunzo ya Kikosi cha Ulinzi na Usalama cha chama hicho (Red Brigade), kwa vijana 200 wa  Kanda ya Kati pamoja na Kikosi maalum cha Karate.

           “Katika  uchaguzi huu hatutaki  kulalamika tena kwamba tumeibiwa kura na tutahakikisha  tutaomba  kura kwa wananchi na tutazilinda,” alisema Mbowe.

         Alisema endapo watakubali kuibiwa kura maana yake hawapo tayari kuongoza.

         Mbowe aliwataka  vijana hao wa Brigade kutokukilinda chama peke yake bali pia kiwe chachu ya ulinzi kwa jamii inayowazunguka kwenye maeneo yao.

            Alibainisha kuwa Chadema  kitaendelea kutoa mafunzo ya ulinzi kwa vijana nchi nzima.

           "Vijana  hawa lazima wajenge moyo wa kujitolea, chama kilijengwa na watu wenye moyo huo ambao baadhi walipata madhara mbalimbali ikiwamo kupoteza maisha,” alisema Mbowe.

             Alisema wajenge sifa ya kuwa wakombozi wa Taifa na  malipo mengine siyo lazima walipwe hapa duniani bali  watapata  kwa Mungu.
Taarifa muhimu kuhusu chadema nyingine soma hapoa chini

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeamua kutumia mabaraza yake kufanya mashambulizi ya kisiasa kujiimarisha miongoni mwa makundi maalum katika jamii.

Kwa mujibu wa habari zilizopatikana kutoka ndani ya chama hicho, chama hicho sasa kitayatumia mabaraza yake ya Vijana (Bavicha), Wanawake (Bawacha) na (Bazecha) kama mkakati wa kulenga makundi mahsusi ya wapiga kura katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu.

Habari hizo zilisema kuwa chama hicho kiliyaagiza mabaraza hayo tangu mwaka jana kuhakikisha yanahamasisha makundi maalum katika jamii na  kuwa mstari wa mbele kwenye mapambano ya kisiasa ya chama hicho.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa chama hicho, Tumaini Makene, alipoulizwa juu ya taarifa hizo,  hakukubali ama kukanusha.

Makene alisema anachofahamu viongozi wakuu wa chama hicho wametawanyika sehemu mbalimbali nchini kwenye shughuli za kukijenga chama.

“Kama unavyojua, hatujawahi kupumzika tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, tumekuwa tukibadili gia na kuongeza umakini kadiri ya matakwa ya safari ya kisiasa ambayo inazidi kushuhudia Chadema na upinzani kwa ujumla ikizidi kuungwa mkono huku Chama Cha Mapinduzi (CCM), nacho kikijaribu kupambana na sisi kwa kutafuta mlango wa kutokea,” alisema Makene na kuongeza:


“Lengo la viongozi hao wakuu kutawanyika nchi nzima ni maandalizi mahususi kwa ajili kuwapatia fursa viongozi hao kushughulika na masuala makubwa ya kukiandaa chama ili kishinde na kushika dola kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu.” Makene alisema mwishoni mwa wiki iliyopita,  Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alikuwa Shinyanga kufunga mafunzo ya uzalendo na ukakamavu kwa vijana na kufanya mkutano wa hadhara Solwa pamoja na kuendesha vikao vya kuimarisha mikoa ya Kanda ya Ziwa Mashariki.

Hakuna maoni