Zinazobamba

EXLUSIVE-GAZETI LA MBOWE LABOMOREWA,MHARIRI WAKE ATIMKA,KUBENEA ACHEKELEA SOMA HAPA KUJUA


Freeman Mbowe



PIGO limelikumba Gazeti la Tanzania Daima baada ya Mhariri wake muhimu  Edsoni Kamukara kuhama Rasmi Gazeti hilo Anaripoti KAROLI VINSENT Endelea nayo
         Taarifa za kuaminika ambazo mtandao huu umezipata zinasema Mhariri huyo ametimkia kwenye Gazeti linalotoka mara moja kwa wiki Gazeti la Mawio.


Pichani ni Edsoni Kamukara
      Chanzo chetu muhimu kutoka kwenye Gazeti la Tanzania Daima ambalo linamilikiwa na Familia ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendelea Chadema Freeman Mbowe amesema mhariri huyo amewaaga waandishi wa gazeti hilo pamoja na wahariri wenzake huku akishindwa kuwaambia sababu ya kuhama kwake.

         “ni kweli Kamukara amehama kwenye Gazeti letu na ametuga jana kwenye kikao,na hata sisi tumesikitika sana kuondoka kwake maana ni mtu muhumi sasa,ukizungumzia watu muhimu sana walioleta mafanikio gazeti letu lazima umtaje kamukara na sijui kwanini kaondoka maana itatuletea pengo kubwa sana”kimesema chanzo chetu.
       Kutimkia huko kwa Mhariri Kamukara kunakuja wiki chache baada ya aliyekuwa mhariri mtandaji wa Gazeti hilo Ansbert Ngurumo kuondoka na kutokana na   y eye kujiingiza kwenye masuala ya siasa,nafasi yake kuchukuliwa na Neville Meena.
Mbali na Ngurumo wahariri wengine waliohama ni Amana Nyembo ambaye alikuwa mhariri wa Makala naye pia ametimkia Gazeti la mwananchi na kuwa Mhariri pia yaani (Sub-editor).

            Wadau wahabari wanena.
Wadau mbalimbali wa masuala ya habari waliozungumza na mtandao huu wameonyesha masikitiko yao makubwa, baada ya kuondoka huko kwa mhariri huyo na kusema ni pengo kubwa kwenye gazeti hilo bora linalotoka kila siku.
       “Mchango wa kamukara ni kubwa sana katika gazeti hili,leo hata mimi mwenyewe nilikuwa nafurahi sana kusoma makala zake na hata Gazeti la Jumatano ambalo yeye analihariri, yaani utagundua huyo mtu anakitu kimoja tofauti sana na wahariri wengine hapa nchini”alisema msomi mmoja wa Shahada ya Habari kutoka chuo KIkuu cha Mlimani
Kwa upande kiongozi mwengine kutoka ndani ya Idara ya Habari Maelezo ambaye akutaka jina lake litajwe mtandaoni alisema Gazeti hilo litakuwa na changamoto kubwa sana kwa utendaji wa Mhariri wake Mtendaji wa sasa,
        Kuhamia huko kwa kamukara kwenye Gazeti la Mawio ambalo linamilikiwa na Aliyekuwa Mhariri Mtendaji  wa Gazeti la Mwanahalisi, Lilofungiwa na Serikali kwa mda usiojulikana Saed Kubenea na kushirikiana na Mkurugenzi mmoja wa Fedha kutoka ndani ya Chadema jina tunalihifadhi ,kunatajwa ni njia ya kulifanya gazeti la Mawio kuzidi kuwa juu.
        Gazeti la Mawio ni miongozi mwa magazeti yanayofanya vizunri sokoni,kwa mujibu wa utafiti uliofanya na mtandao wa HABARI24.blogs,umelitaja gazeti hilo kuwa ni gazeti linalouza nakala myingi kwa upande wa magazeti yanayotoka mara moja kwa wiki.

Hakuna maoni