AMKA ASUBUHI NA HABARI NJEMA KUTOKA MANISPAA YA ILALA,SOMA HAPA KUJUA
Pichani ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala Issaya Mussa akizungumza na waandishi wa Habari Jijin Dar Es Salaam picha na Seleiman Magari |
Na Karoli
Vinsent
KATIKA
jitihada ya kupambana na Tatizo la Msongamano wa Magari katika Jiji la Dar Es
Salaam,Manispaa ya Ilala na Temeke kwa kushirikiana na Kampuni toka china
imeanza ujenzi wa barabara ya kisasa ambayo itaanzia Uwanja wa Ndege Jijin Dar
Es Salaam kupitia Banana,kitunda ,msongora hadi Chamanzi Wilaya ya Temeke.
Hayo yamesemwa Jana na Mkurugenzi wa
Manispaa ya Ilala,Issa Mussa wakati wa Mkutano na Waaandishi wa Habari Jijini
Dar es Salaam,ambapo alisema Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita 12.8 ambayo
itakuwa na njia sita itawasaidia wakazi wa Dar es Salaam katika kupunguza
Tatizo sugu la msongamano wa Magari.
“Barabara hii itawasaidia sana wakazi wa
Wiliya hizi mbili ambazo barabara hii inapita ambazo wilaya yangu
ninayoinongoza ya Ilala pamoja na Temeke,kwani kumekuwa na Tatizo kubwa sana
kwa wakazi wa Wilaya ya Temeke kutoka Chamanzi kuja uwanja wa Ndege ambapo
awali iliwalazimu kupitia njia ndefu na kukaa sana kwenye barabarani lakini kwa
ujenzi huu wa barabara wa Njia sita ukikamilika utaweza kuwaondolea Adha wakazi
wa Wilaya hizi mbili”alisema Mussa.
Mussa alizidi kusema kuwa mradi huo wa
barabara umeanza rasmi mwezi wa nne mwaka huu kwa hatua za mwanzo za kufanyia
tasmini ikiwemo maripo ya Fidia kwa wakazi ambao barabara hiyo itapita na
kusema mradi utagarimu pesa za kimarekani Bilioni biloni 64 na pesa hizo zote
ni kwa msaada wa Kampuni toka china na utarajia kukamilika mwezi 10,2016.
“Kumbukeni barabara hii inajengwa kwa
msaada wa Kampuni toka china ambayo ndio itakayosimamia ujenzi wote wa barabara
hii na wao waneiomba serikali iwaondolee kodi tu wakati wa kuleta Vifaa vyao
ambavyo vitatumika katika ujenzi wa mradi huu na Barabara hii imepewa Jina la “Kikwete
Frendship Highway”alisema mkurugenzi Mussa.
Vilevile Mussa alizidi kusema mradi wa
barabara utakapoishia maeneo ya Chamanzi kutajengwa “Busneess Park”kubwa
yakiwemo maduka makubwa ya Biashara ambayo yatamilikiwa na Kampuni ambayo
imesaidia kujenga barabara hiyo na kuongeza kuwa maduka hayo yatasaidia
kuwainua kipato wakazi wa Chamanzi na sehemu zengine.
Aidha
Mkurugenzi huyo akawataka wananchi kuupokea mradi huo kwa furaha kubwa na kuwa
tayari kushirikiana na maafisa ambao
watakuja kutasmini nyumba ambazo zitapitiwa na mradi huo ili wapewe Fidia
Hakuna maoni
Chapisha Maoni