Zinazobamba

LHRC CHAWAPIGIA MAGOTI SERIKALI,KISA NI UTAPELI UNAOFANYWA WAKOPESHA FEDHA DHIDI YA WAJASILIAMALI,

Adv. Flaviana Charles (KULIA) akionyesha ripoti ya haki za binadamu, Adv. Charles leo amemulika idara ya ujasiliamali na kusema kuwa sekta hiyo imesahaulika na kwamba watanzania wengi wamekuwa wakitapeliwa kutokana na uelewa mdogo wa kisheria na mikopo isiyo na tija
 Kile kinachodaiwa kuwa ni dhuruma , wizi na utapeli uliokithiri unaofanywa na taasisi za kukopesha fedha  hapa nchini umewasukuma kituo cha sheria na  haki za binadam kuitaka serikali  kuandaa mazingira ya kuwadhibiti taasisi hizo ili wasiweze kuendelea kuwatapeli maaelfu ya wajasiliamali,

Hatua hiyo imekuja kufuatia viliyo vya wajasiliamali katika mikoa ya Arusha, Meru na Babati ambao wamekusanya zaidi ya kesi 26 katika kituo Cha arusha wakiwatuhusu mashirika hayo yanayojihusisha na ukopeshaji wa fedha kufanya utapeli wa waziwazi kwa raia hao,

Akizungumza na waandish wa habari mapema hii leo, Kaimu mkurugenzi wa mradi wa kazi za staha kwa wananchi waliojiari katika sekta zisizo rasmi, Adv. Flaviana Charles amesma katika mradi huo wamegundua uatapeli wa hali ya juu unaofanywa na mashirika yanaojihusisha na kukopesha fedha kwa wananchi, huku utapeli mkubwa ukifanywa kwa njia ya mikataba ya kinyonyaji,

Charles, ameendelea kufunguka kuwa,katika mradi huo uliowashirikisha jumla ya wajasiliamali 775, umeonyesha mafanikio makubwa sana kwa kubaini changamoto mbalimbali za
wajasiliamali, ambazo kama serikali hatakuwa makini nazo basi tunatengeza bomu kubwa ambalo likifumka hakuna atakae pona,

Mradi huoa ulitumia kipindi cha miaka mitatu katika mikoa hiyo ya kanda za kaskazini, umebaini uhitaji wa hali ya juu kwa nguvu za serikali kuingilia kati mifumo mibovu  ya taasisi za kukopesha fedha ambayo imekuwa ikiwanyonya wajasiliamali hapa nchini,

Katika kuondoa tatizo la utapeli linalofanywa na taasisi za kifedha ambazo zimepewa dhamana ya kukopesha wajasiliamali, Kituo kimependekeza uundwaji wa haraka wa mamlaka  ya kuthibiti taasisi za mikopo hapa nchini, ili mashirika ya mikopo waweze kutoa mikopo yenye riba nafuu na masharti rahisi kwa wajasiliamali wa kitanzania

Watu wamekuwa wakitapeliwa, na unakuta taasisi zingine hazijasajiriwa kabisa, lakini bado zinaendesha shughuli za ukopeshaji na hata zile ambazo zimesajiriwa bado zinatengeneza mikata ambao ni mizito kuisoma hivyo mali nyingi za walala hoi zinataifishwa kutokana na kutoelewa kwa mkata husika ama kushindwa kulipa riba ambayo amewekewa,Alisema  Flaviana

Naye kwa upande wake meneja mradi wa kazi za staha kwa wananchi waliojiajiri katika sekta isiyo rasmi, Bw.Hussein Sengu amebainisha changamoto mbalimbali ambazo wamekuwa wakikumbana nazo katika utekelezaji wa mradi huo uliofadhiliwa na umoja wa Ulaya (EU) ambapo katika kazi hiyo walishirikiana kwa karibu na shilika la kijerumani linalohuska na idadi ya watu ulimwenguni Deutsche stiftung weltbevoelkerung (DSW) , kuwa matatizo makubwa ni vilio vya wajasiliamali ambao wamekuwa wakitapeliwa mali zao na kuacha makazi yao huku serikali likifumbia macho suala hilo.

Unakuta watu wanakufuata kwa upendo kabisa kuwa kunapesa lakini, mwisho wa siku ni vilo kwani masharti ni magumu na yasiotekelezeka hatua inayowafanya watu wengi kupoteza mali zao za thamani kwa pesa ndogo waliochukua kujianzishia biashara wenyewe,

Taasisi ya ujasiliamali inaajiri takribani asilimia 60 ya watanzania wote, hivyo kitendo cha kuacha tasnia ya ujasiliamali kuwa haina mwenyewe ni hatari kwa mustakali wa taifa letu, Aliongeza Sengu wakati akifafanua utapeli unaofanywa na mashirika ya kukopehs afedha kwa wajasiliamali .

HAYA NDIYO MAPENDEKEZO YA KITUO KAMA KWELI TUNATAKA KUWANASUA WAJASILIAMALI:

·         Serikali iunde mamlaka ya kudhibiti tasnia ya ujasiliamali, kwa kuzidhibi taasisi za mikopo isiende nje ya sera ya mamlaka  itakayoundwa

·         Watunga sera watunge sra zitakazoweka misingi ya sekta sisizo rasmi

·         Serikali ijipime na kuanza kuangalia sekta ya ujasiliamali na kuweka mifumo ili kuondoa dhuluma, wizi na utapeli unaoanza kukua kama uyoga katika taasisi za kukopesha fedha

MWISHOO


Maoni 1

HELEN KIJO-BISIMBA alisema ...

Hii ni muhimu kabisa kwani wajasiriamali wa najaribu kujikwamua kiuchumi wakati wakichangi apat la taifa , nguvu zao hupotea iwapo watatapeliwa.
HELEN