Zinazobamba

Mbeto:Hotuba ya Rais Mwinyi akifunga Baraza la Wawakilishi zbar ni ya kimapinduzi


Na Mwandishi  Wetu, Zanzibar 

Chama Cha Mapinduzi  kimesema hotuba ya Rais wa Zanzibar   Dk Hussein Ali Mwinyi   kabla ya kulivunja  alioitoa  kabla ya kuvunja  Baraza la Wawakilishi  Zanzibar (BLW) ni ya  kujivunia ufanisi wa sera na mkakati wa maendeleo ya kimapinduzi .

Chama hicho pia kimeitaja hotuba  hiyo licha ya kugusa sekta muhimu na utendaji  wa  kazi za serikali,  imeonyesha kupanda grafu ya maendeleo katika sekta za umma na sekta binafsi . 

Katibu  wa Kamati  Maalum  ya NEC  Zanziabr , Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo  , Khamis  Mbeto  Khamis,  amesema licha SMZ kufanya  mageuzi ya kimapinduzi,  Serikali kwa miaka mitano iliopita , imeleta  tija kwa maendeleo yaliofikiwa.

Mbeto  alisema utekelezaji wa kisera kwa miaka mitano toka  mwaka  2020 -2025, SMZ imejiegemeza  zaidi katika kukuza sekta za  Utalii, Viwanda, Kilimo na Michezo na kasi ya   ukuaji Uchumi wa Bluu ,pato la mtu na mapato ya Taifa .

Alisema kwa miaka mitano  iliopita ,  SMZ  chini ya  Rais  Dk Mwinyi,  imefanikisha malengo ya kisera  katika   sekta za Elimu,   Uwekezaji, Viwanda, Afya , Kilimo, Maji,Uvuvi na Biashara, Ajira ,Usafiri wa Anga na Tumefanikiwa kugawa vitalu kwa Makampuni ya Uchimbaji wa Gesi na Mafuta.

"Hotuba ya Rais Dk Mwinyi imewafumbua macho na masikio Wanasiasa  wenye hulka ya ujuvi na ukaidi .Kila mtu amesikia mambo yaliofanikishwa na SMZ kwa miaka mitano iliopita  "Alisema Mbeto 

Aidha  hotuba  hiyo imetaja hatua zilizochukukiwa  kimkakati lakini pia kuelezea matarajio na  kufikia malengo mahususi kwa miaka mitano ijayo kuanzia  mwaka  2025 hadi 2030 .

" CCM  imeridhishwa kwa kiasi  kikubwa na mkakati wa utendaji na utekelezaji wa kisera chini ya Awamu ya Nane. Chama kina  imani  kubwa na  uongozi wa  Rais  Dk Mwinyi   na watendaji wa Serikali  yake " Alisisitiza Mbeto 

Pia Katibu  huyo Mwenezi  ,alisema CCM  kimefurahishwa kwa hatua madhubuti za  SMZ za kuendeleza  Umoja wa Kitaifa, kupinga  ubaguzi  wa aina yoyote na  kutilia mkazo dhima ya kuwaunganisha wananachi.

Mbeto  alisema ni aibu  kubwa kwa Wanasiasa ambao  mara kadhaa, wamekuwa wakipotosha  ukweli  wa mambo na kudaii hakuna kilichofanywa na SMZ kwa miaka mitano  iliopita .

"Yote yalioahidiwa kisera na Rais  Dk Mwinyi  wakati  wa kampeni za  mwaka 2020 ametimiza ahadi zake .Ni kawaida ya CCM kuahidi na kutekeleza  kupitia Ilani ya Uchaguzi  ya Mwaka 2020/2025" Alielez

Katibu Mwenezi  huyo alisema kutokana na kupatikana na ufanisi wa kisera uliofanyika miaka mitano iliopita, CCM  ina hakika ya kushinda tena uchaguzi   Zanzibar ifikapo oktoba mwaka huu.

No comments