MWAKIPOSA AFUNGUKA MIAKA MITATU YA RAIS DKT.SAMIA MADARAKANI.
Na Mussa
Augustine.
Mwenyekii
wa Mtaa wa Dovya Kata ya Bunju Manispaa
ya Kinondoni Anasisye Lazarus Mwakiposa amesema kuwa miaka Mitatu ya Uongozi wa
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan Mtaa huo umetekeleza Vyema Ilani ya Chama Cha
Mapinduzi(CCM) katika kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa zinawakabili Wananchi.
Mwakiposa
amesema hayo wakati akizungumza na kituo hiki nakubainisha kuwa Mtaa wa Dovya hapo
awali haukua na maeneo ya kujenga kituo cha polisi,shule,Zahanati,Ofisi ya
Serikali ya Mtaa,lakini katika uongozi wa Rais Dkta Samia maeneo hayo
yamepatikana.
Mwenyekiti
huyo wa Wenyeviti wa Serikali za Mtaa Manispaa ya kinondoni ambaye pia ni Kaimu
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa serikali za Mtaa Mkoa wa Dar es salaam amebainisha kuwa hadi sasa Barabara nne zimejengwa kwa
kiwango cha lami,pamoja na Daraja moja ambalo limejengwa kwa kiasi cha shilingi
milioni 434,huku pia Mfereji wa
kuchepusha maji umejengwa na kuondoa athari ya mafuriko kwa wananchi.
Amezitaja
Barabara hizo kuwa ni pamoja na barabara ya Makala-JKT
Mbweni,Umoja,Burumawe-Kairuki pamoja na Shemdoe nakusema kuwa hapo awali
wananchi walikuwa wakichangishana fedha kukarabati barabara hizo.
“Miaka
mitatu ya uongozi wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan ni miaka ya kumbukumbu ya
Maendeleo Makubwa kwenye mtaa wangu wenye wakazi wapatao elfu kumi na mbili (12000),lakini
bado kuna changamoto kadhaa ambazo wananchi wanaomba zitatuliwe mapema”amesema
Nakuongeza
kuwa “Changamoto hizo ni pamoja na Ujenzi wa barabara ya Magereza-National
Housing ,na Matumaini Sobers House ,hata hivyo ndani ya miaka minne ya uongozi
wangu kama mwenyekiti wa serikali ya mtaa huu nimefanya mengi ikiwa ni pamoja
na kujenga ofisi mpya pamoja na kupata eneo la ujenzi wa shule ya Boko Dovya
hivyo naomba Manispaa itenge fedha kujenga shule hiyo”.
Mwakiposa
ametumia fusra hiyo pia kumuomba rais Samia kuwajengea shule yenye mchepuo wa Kiingereza
yaani Dovya Primary School and English Medium ili watoto wasihangaike kwenda
kusoma mbali na mtaa huo.
Aidha
ameomba pia kujengwa kwa Zahanati na Barabara ya Maendeleo,Boko –Magereza kwenye
kiwango cha lami kwani kwa sasa zipo katika kiwango cha Changarawe.
Katika hatua
nyingine Mwenyekiti huyo wa Serikali ya Mtaa Dovya amekemea vitendo
vinavyofanywa na baadhi ya Watu kuwatukana viongozi kupitia mitandao ya
kijamii.
“Mamlaka ya
Mawasiliano Nchini(TCRA) iwachukulie hatu wale wote wanaohusika ,mmomonyoko wa
maadili ndio unaochangia mtu asiwe na heshima kwa mtu anaemzidi umri au
cheo,Mh.Rais Dkt Samia halali kwasababu ya watanzania lakini kuna baadhi ya
watu wanajitokeza na kumtukana ,TCRA isilale iwachukulie hatua za kisheria”amesisitiza
Mwakiposa.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni