Zinazobamba

Sakata la mchakato wa mabadiriko ya katiba… LHRC wataka mabadiriko ya muundo wa Bunge Maalum la katiba

 

Mwandishi wetu

 


KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimetoa maoni ya namna bora ya kuendelea na mchakato wa kupatikana kwa Katiba Mpya.

 

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 24, 2022 jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Wakili Anna Henga Ametaka kufanyika mabadiliko ya Sheria yote ya mabadiliko ya Katiba Na. 8/211 na kuweka muundo mpya wa Bunge Maalum la Katiba ili kuanza majadiliano na kutunga Katiba Mpya. 

 

“Bunge hilo litumie Rasimu ya Pili (II) ya Katiba. Hii inatokana na ukweli kwamba, kulikuwa na mjadala mkali kuhusu upatikanaji wa Katiba Pendekezwa, 2014,” amesema Wakili Henga.

 

Akizungumzia kuhusu faida ya njia hiyo, amesema kwamba endapo Bunge Maalum la Katiba litaundwa kwa kuweka uwakilishi mpana wa wananchi zaidi ya wabunge kutarudisha imani ya wananchi juu ya mchakato wa katiba na kuwapa uhakika kuwa, masuala ya wananchi yanazingatiwa vyema tofauti na kutanguliza zaidi maslahi ya baadhi ya wanasiasa. 

 

Pia, amesema njia hii itajenga maridhiano na kupunguza tofauti zilizopo kati ya wananchi na viongozi wa siasa. 

 

“Aidha ni muhimu kukumbuka kuwa mchakato wowote wa kufanya mabadiliko ya katiba ni lazima kuwepo kwa uhuru wa wananchi kushiriki, kuafikiana na kumiliki mchakato wa kuandika katiba, kwani Katiba inapaswa kutokana na ushiriki mkubwa wa wananchi,” ameongeza Wakili Henga.

 

Hivyo Wakili Henga ametoa wito kwa Serikali Kupeleka muswada wa mabadiliko ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ili kuunda upya Bunge Maalum likiwa na uwakilishi tofauti na wajumbe tofauti na wabunge wachache wa vyama vyote wanaoweza kuwakilishwa.

 

Vile vile Serikali ipeleke mswada wa mabadiliko ya Sheria ya Kura ya Maoni ili kuipa uhalali wa kisheria sheria hii.

 

Aisha Bunge Maalum la Katiba litakaloundwa litumie Rasimu ya Pili (II) ya Katiba katika majadiliano yake.

Kadhalika Serikali iendelee kufungua milango ya majadiliano miongoni mwa watanzania kwa njia ya mikutano, makongamano, midahalo na vyombo vya habari juu ya mambo ya msingi na muhimu ndani ya katiba kwa mstakabari wa taifa letu.

 

No comments