Zinazobamba

Simbaulanga awakumbusha Wakristo, Waislam kuepuka migogoro ya kidini.

Na Mussa Augustine.

Mtumishi wa Mungu Cecil Simbaulanga amewakumbusha waamini wa kikristo na Waislam nchini kuepuka kujiingiza kwenye migogoro ya kidini na badala yake wapendane na kushirikiana katika kulijenga taifa kiimani.

Hayo ameyasema wakati wa mahojiano na Mtandao huu, ambapo amesema kwamba amefanikiwa kuandika vitabu vinavyotoa mafundisho ambayo wakristo na waislamu wamekua yakiwachanganya nakushindwa kusimamia imani zao.

Simbaulanga amesema kwamba ameandika kitabu kiitwacho "Chanzo cha Mihadhara ya Kidini Tanzania" ili kujibu mihadhara na kuelimisha wakristo ambao walikua wakiulizwa maswali kwenye mihadhara wanashindwa kujibu kutokana na kutokua na uelewa mpana juu ya maandiko ya dini.

"Mwaka 1986 Tanzania iligubikwa na mihadhara yakidini iliyoendeshwa na  waislam  wakitumia Quran takatifu  na Biblia takatifu ambapo mlengo wa mihadhara hiyo ilikua ni kuwahoji wakristo juu ya imani yao, mihadhara hiyo ilishamiri  hadi mwaka 1992 ndipo nilipoguswa na kuanzisha kikundi cha kujibu mihadhara hiyo" amesema \

Kikundi hicho nilikiita "Biblia ni Jibu"ambapo toka kipindi hicho hadi mwaka 2021 hali ipo shwari kunamahusiano mazuri kati ya wakristo na waislam, wakristo wanauwezo wa kujibu masuali kutoka kwa waislam, ndipo nilipoamua kuandika kitabu hiki ili wajue namna mihadhara yakidini ilivyoanza" ameongeza Simbaulanga.

Pia ameendelea kusema kuwa amefanikiwa kuandika kitabu kingine alichokiita "Nani mmiliki halali wa mji wa Yerusalem na Nchi ya Israeli"? Waisrael au Wapelestina?  Je Biblia takatifu na Quran tukufu vinasemaje? hii ni baada ya kushuhudia makongamano mbalimbali ambayo yalifanywa na waislam hapa nchini mwaka 2004.

Amesema kwamba vitabu vyote vya Quran takatifu na Biblia vinaelezea uhalisia wa umiliki halali wa Mji wa Yerusalem nakwamba  Nchi hiyo ni Israel kwahiyo waumini wa dini ya kiislam na  wakristo wanaweza kupata nakala ya kitabu hiki ili waweze kujisomea nakujua mambo mengi.

"Naomba kuwasihi waamini wa kiislam na wakristo wenzangu kuacha kuingiza migogoro ya kugombana juu ya mashariki ya kati mwamuzi wa kweli ni kufuata kwenye vitabu vitabu takatifu yaani Quran takatifu na Biblia takaptifu" amesema 

" Wakristo na waislam wapate nakala za vitabu hivi wajisomee vitawasaidia kuondoa sintofahamu iliyopo ,hivyo watu wenye mapenzi mema wajitokeze kunisaidia nina changamoto ya ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuchapisha vitabu hivi vipatikane kwa wingi,atakaeguswa awasiliane nami kupitia namba yangu ya Whatsap 0789606070" ameongeza  mtumishi huyo wa Mungu.

Hakuna maoni