Zinazobamba

MAGAIDI WAITESA NCHI YA KENYA,SOMA HAPO KUJUA


Jeshi la Polisi nchini Kenya limepoteza Askari wake watano baada ya gari lao kukanyaga bomu lililotegwa barabarani katika mji wa Liboi karibu na mpaka na Somalia.

Polisi hao wameuawa na shambulio lililotokea katika eneo ambalo Polisi wengine wanne waliuawa katika shambulio kama hilo lililotekelezwa na kundi la Alshabab hivi karibuni.

Wapiganaji wa kundi la Al-Shabab ambao makao yao makuu ni Somali, wameendelea kufanya mashambulio kadhaa nchini Kenya katika siku za hivi karibuni, wakiitaka Serikari ya Kenya kuondoa majeshi yake yanayofanya kazi katika vikosi vya AMISOM.